Saturday, 19 November 2016

Jipime ufahamu wako kiblia!

KWA WASOMI WA BIBLIA TUCHANGAMSHE BONGO ZETU.

1. Fundisho kuu la Biblia ni nini?
A Watu watende matendo mema
B. Wokovu kupitia kwa Yesu Kristo.
C. Wokovu ni neema tu.

2. Biblia ni tofauti na vitabu vingi. Moja ya tofauti hizo ni.
A. Ganda la juu ya biblia ni jeusi tu.
B Biblia ni kitabu kilichotafsiriwa kwa lugha nyingi kuliko kitabu chochote.
C Biblia ni kitabu kikubwa zaidi ya vitabu vingine.

3 Biblia iliandikwa kwa miaka mingapi hadi ikakamilika?
A 1500
B 1569
C 1600

4 Nani mwandishi wa Biblia.
A. Musa na manabii wengine.
B Manabii, makuhani, mitume na wafalme.
C. Roho mtakatifu kwa kuwatumia watu.

5  Vitabu vya agano la kale vimegawanyika katika makundi makuu mangapi?
A. 4
B. 2
C. 6

6. Vitabu vya agano jipya vimegawanyika ktk makundi makuu mangapi?
A. 4
B. 3
C. 6

7. Mtume Paulo peke yake ameandika vitabu vingapi kwenye Biblia?
A. 21
B. 13
C. 16

8. Mtume Yohana ameandika vitabu vingapi kwenye Biblia?
A. 1
B. 4
C. 5

9. Nani mwandishi wa kitabu cha matendo ya mitume?
A. Paulo
B. Luka
C . Timotheo

10. Kabla ya mtume Mathayo  hajaitwa na Yesu amfuate, alikua anafanya kazi gani?
A. Mtoza ushuru.
B.Mvuvi
C. Mfanya biashara.

11. Nini maana ya Biblia …………… ...................…………………………………………

12. Nini maana ya Kristo ……………………………………………………………………

13. Nini maana ya jina la Petro ……………………………………………………………………

14. Yesu alizaliwa ktk mji unaoitwaje?
……………………………………………………………………

15. Ni farisayo yupi aliyemfuata Yesu nyakati za usiku akiogopa asionekane na wayahudi?
……………………………………………………………………

16. Kulingana na injili ya Yohana, muujiza wa kwanza aliofanya Yesu ulikua ni upi?
…………………………………………………………………

17. Yesu baada ya kufufuka, alendelea kukaa duniani kwa siku ngapi?
…………………………………………………………………
18. Nani aliyembatiza kwa maji mtume Paulo?
…………………………………………………………………

19. Unafikiri ni sababu gani ilimfanya Ibrahimu aitwe " Baba wa Imani"?

20. Kwa nini  Mungu aliwachelewesha Israeli kuvuka jangwani?

******* MWISHO*****

Thursday, 17 November 2016

Chagua kunyamaza uwapo na hasira!!

          CHAGUA KUNYAMAZA

MITHALI 11:12 Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

MITHALI 17:28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.

Changamoto kubwa tuliyonayo ni kwamba tunataka kuongea kila wakati, tunataka kujibu kila tunachokisikia, kila tunachokiona tunataka kukisemea kitu.

Kuna wakati tunasikia na kukutana na mambo ambayo kiuhalisia moyo unagoma kabisa kunyamaza, unatamani ujibu, unatamani uwaambie watu yale umefanyiwa, unatamani uelezee vile umeumizwa lakini kumbe si kila jambo linatakiwa kuongelewa.

Si kila ukionacho unatakiwa kukisemea kitu. Si kila usikiacho/uambiwacho ni lazima ujibu.

Si kila ufanyiwacho ni lazima umwambie kila mtu.

MUHUBIRI 3:1 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

       Ipo nguvu katika kunyamaza

Yapo mambo ambayo tunapaswa kuongea, kusema, lakini yapo mambo ambayo tunapaswa kunyamaza kwa ajili ya usalama wa Roho zetu.

Ni kweli kuna wakati unasemwa sana vibaya, unasingiziwa, unatukanwa nk nk, lakini ni lazima ukumbuke kwamba kuna mazingira ambayo hupaswi kujibizana hata kama umeumia kiasi gani.

              Unajua ni kwanini?

Ukisemwa vibaya, ukitukanwa, ukidharauliwa lazima moyo utaghafilika, moyo ukighafilika lazima utakuwa na hasira na ghadhabu.

Ukiwa na hasira katu usitegemee kuwa utajadiliana na mtu kwa hekima.

Ukiongea utaongea katika uwepo wa hasira, ukijibu utajibu kulingana na kiwango cha hasira ulichonacho.

Sasa jiulize majibu yanayotoka kutokana na msukumo wa hasira huwa yanakuwaje?

Mazuri? Ya upole? Ya hekima? Ya unyenyekevu? I am sure jibu ni hapana.

Kama jibu ni hapana that means utaongea vitu vibaya ambavyo ni chukizo kwa MUNGU kwa sababu amesema maneno yetu na yakolee munyu (chumvi).

Sasa badala ya kuongea upumbavu na ukamkosea MUNGU kwanini usichague kunyamaza?

AMOSI 5:3 Kwa ajili ya hayo mwenye busara atanyamaza kimya wakati kama huo; kwa kuwa ni wakati mbaya.

Nimekuwa inspired sana na mwanamke Abigaili, ni kweli mumewe alikuwa na makosa, ni kweli alikuwa mlevi, lakini mwanamke huyu alijua ni wakati gani, na mazingira gani alipaswa kuongea na mumewe na alijua aongee nini. Alipomkuta mumewe yupo katika hali ya ulevi, ALINYAMAZA, alijua kuwa huu sio wakati wa kusema jambo lolote.

1 SAMWELI 25:1

Ni vyema sisi pia tukajifunza kusoma mazingira na nyakati na hali za watu zilivyo ili tujue ni wakati gani tujibu, tuongee nini na ni wakati gani tunyamaze

Kilinde kinywa, hakikisha haukiachi kinene mabaya – ZABURI 50:19.

Usipoteze marafiki na kuharibu mahusiano kwa ajili ya kinywa kibovu – MITHALI 11:9.

Ni vyema tukajifunza kujua ni neno gani tukitamka kwa wakati/hali/mazingira gani litakubaliwa –MITHALI 10:32.

ZABURI 19:14 – Bwana na akafanye maneno yetu yakapate kibali mbele zake MUNGU na mbele za wanadamu pia.

1SAMWELI 25:36

Umeumizwa, umekwazwa, umetukanwa, umedharauliwa, KATIKA MAZINGIRA YA HASIRA NA GHADHABU JITAHIDI KUNYAMAZA.

Ni kweli moyo na akili na hisia vinakusukuma kujibu, kubisha n.k, lakini elewa impact za kujibizana ukiwa na hasira na hizo ni bora ukae kimya.

AKUSHINDAE KUONGEA, MSHINDE KUNYAMAZA

          Muwe na siku njema!

Sunday, 30 October 2016

Disable Copy and Paste in your blog!

How to Disable Copy Paste In Your Blogg


In internet there are easy way to copy text from your websites and paste it to their site without your permission. There are many blogger site which often doesn't make it possible for us to copy the content on the websites. Admin protected his/her websites post content by pasting code on their websites.

Today,your likely blog  songea computer lab will share a magical tips which protect your content from copy and paste.

Disable Copy Paste in Blogger

Step 1: Go to Blogger

Step 2: Then click on your site and go to Layout

Step 4: After selecting Layout then click on Add a Gadget

Step 5: Then it will open a window and select HTML/JavaScript

Step 6: Then paste following code into the box
<!- www.codiblog.com start disable copy paste --><script type='text/javascript'> if(typeof document.onselectstart!="undefined" ) {document.onselectstart=new Function ("return false" ); } else{document.onmousedown=new Function ("return false" );document.onmouseup=new Function ("return false"); } </script><!-- www.codiblog.com End disable copy paste -->Step 7: Now Save the open window and done.

Now see your site and you can not copy your post content. That's it. Happy Comment & share on This Post! on your result that have been checked





Monday, 24 October 2016

Vyakula vinavyo ongeza hamu ya kufanya tendo la ndoa!

Tatizo la uwezo wa kufanya tendo la ndoa linazidi kukua miongoni wa wanandoa na wapenzi wengi. Takwimu za kitafiti zinaonyesha kuwa karibu ndoa 4 kati ya 10 zenye umri wa miaka 3 na kuendelea zinakabiliana na tatizo hili. Aidha wanaume 6 kati ya 10 wanatajwa kulalamikia upungufu wa nguvu za kiume.

Pamoja na matatizo mengine kutajwa kuchangia upungufu wa nguvu za kiume na kushuka kwa msisimko wa tendo miongoni mwa wanandoa, uchunguzi umeonesha kuwa utumiaji holela wa vyakula hasa vyenye mafuta ni moja kati ya sababu zinazochangia kwa kasi tatizo hili.

Kwa kuzingatia hilo, watafiti wa masuala ya uhusiano wa kimapenzi wamebaini aina mbalimbali ya vyakula ambavyo vina uwezo wa kumuongezea mtu nguvu ya kufanya tendo la ndoa.  Vyakula hivyo ni hivi vifuatavyo:

1. PILIPILI
Kama tunavyojua wote mara nyingi chakula ambacho kimeungwa pilipili hufanya hata mapigo ya moyo kuwa tofauti na wakati mwingine hata jasho au kamasi hutoka. Ndani ya pilipili kuna kitu kinaitwa capsaicin ambacho hufanya pilipili iwe na hali ya ukali. Capsaicin huwezesha ubongo kutoa homoni ya endorphins ambayo huleta mgusu wa hisia za raha wakati wa kufanya tendo la ndoa.
Pia pilipili husisimua mfumo wa fahamu (nerves) wa ubongo na katika kufanya hivyo huwezesha kuamshwa haraka kimapenzi (kunyegeka) wakati wa tendo la ndoa na pia ukiguswa au kubusiwa au kunyonywa au kupapaswa unapata hisia kila sehemu ya mwili.

2. MATUNDA NA MBOGA ZA MAJANI 
Ulaji wa matunda na mboga za majani una matokeo makubwa sana katika hamu ya tendo la ndoa kwa njia nyingi. Kwanza matunda na mboga za majani hupunguza kiwango cha mafuta na unene (cholesterol).  Kuongezeka kwa mafuta mwilini huzuia mzunguko wa damu kwa kubana mishipa ya damu.

Pia kula matunda na mboga za majani huhakikisha balance ya uzito kwani unene (obesity) kwa wanaume kuna matokeo mabaya katika kuzalisha homeni za testoeterone na hatimaye jogoo kushindwa kuwika na kuwa na pia mwanaume anakuwa na hisia za mapenzi (libido) kidogo.

Na pia wanandoa wanapozidi kunenepeana ndipo na hali ya kufurahia au kuwa na hamu ya tendo la ndoa huzidi kupungua. Kitalaam inashauriwa kula milo (potions) 3-5 za matunda kwa siku.

3. NAFAKA ZISIZOKOBOLEWA
Nafaka hasa zisizokobolewa kama mahindi, ngano, uwele, nk zina nyuzinyuzi (fibre) na sukari ngumu (complex sugar) ambazo kusaidia kutunza uzito wa mwili. Nafaka husaidia katika kuzalisha homoni za testosterone kwenye damu.

Na pia nafaka huwezesha mtu kuwa na nguvu hatimaye kwenda masafa marefu wakati wa tendo.

Kula nafaka nzima kama vile brown bread badala ya white bread, pia kula nafaka halisi badala ya cornflakes ni jambo zuri linalokuhakikisha afya nejama na mahusiano mazuri ya ndoa yako.

4. TANGAWIZI
Tangawizi ni kiungo cha mboga ambacho husisimua sana na kusaidia mfumo wa mzunguko wa damu mwilini. Tangawizi zinajulikana sana kwa kusukuma damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi yaani uke na uume hivyo kuwa na umuhimu sana katika kuboresha ufanyaji wa tendo la ndoa. Inaweza kuliwa mbichi, au kuliwa ikiwa imeungwa kwenye chakula au kusagwa na kuwa kama unga na kutumiwa kama chai.

5. ASALI
Asali ina madini yanayoitwa boron, ambayo husaidia mwili kutumia homoni ya estrogen ambayo ni homoni inayohusika na viungo ya uzazi na mapenzi kwa mwanamke.

Pia kuna utafiti unaoonesha kwamba asali huongeza nguvu, kitendo ambacho kitapelekea mwanamke kuwa uwezo na hamu ya tendo la ndoa au libido.

6. KARANGA
Karanga huhusika katika kuchochea mfumo wa mzunguko wa damu (vascular system). Mzunguko wa damu ulio sawasawa katika uke na uume huwezesha mwanaume na mwanamke kupata msisimko wa mapenzi haraka hatimaye tendo la ndoa kuwa murua.

Pia karanga zina madini muhimu kama vile magnesium, asidi ya folic na zinc ambayo ni muhimu sana katika usalishaji wa mbegu za mwanaume.

7. CHAZA (OYSTERS) NA PWEZA
Hawa ni aina ya samaki ambao hupatikana katika maji chumvi. Huwa na kiasi kikubwa sana cha madini ya zinc na haya madini ndiyo huhusika zaidi na uzalishaji wa homoni ya testosterone kwa wanaume.

Pia imethibitika kwamba wanaume wenye ukosefu wa madini ya zinc huwa na matatizo ya nguvu za kiume.  Pia madini mengi ya zinc mwilini huongeza kiwango cha shahawa kwa wanaume.

8. SOYA
Pamoja na kuwa na kiwango kidogo sana cha mafuta (fat) na pia kuwa na kiwango kizuri cha protein, soya zina phytoestrogens ambayo husaidia sana wanawake ambao wamefikia menopause kutengeneza homoni estrogen ya ziada.

Husaidia uke kuwa laini (wet, lubricated) mwanamke akisisimuliwa wakati wa tendo la ndoa.

9. CHOKOLETI
Chocolate ina phenylethylamine, kemikali ambayo husababisha hisia (feelings) za furaha wakati wa mwanamke au mwanaume kufika kileleni (orgasm). Inasaidia sana kula chocolate masaa machache kabla ya kuanza kufanya tendo la ndoa.

10. PARACHICHI
Aina nyingine ya chakula ambacho husaidia kuongeza uwezo wa mtu kufanya tendo la ndoa ni Parachichi. Tunda hili linauwezo mkubwa wa kuzalisha vitamini E ambayo husaidia katika uzalishaji wa homoni.

Inatajwa kuwa watu wanaotumia tunda hili kwa wingi huwana msisimko mkali wa kimapenzi na kwa upande wa wanawake husaidia kuongeza majimaji yenye utelezi sehemu za siri na hivyo kuzuia uwezekano wa kuchubuka wakati wa kujamiiana.

Tuesday, 18 October 2016

Nchi mpya kuanzishwa angani!

Wanasayansi hao wanataka kuunda taifa anga za juu ambalo litaitwa Asgardia

Kundi la wanasayansi mjini Vienna, Austria wameanzisha mpango wa kuunda taifa la amani la aina yake ambalo litakuwa na jina Asgardia.

Taifa hilo litaundwa katika anga za juu, eneo.

Maelezo kwenye tovuti ya wanasayansi hao yanasema taifa hilo litakuwa nje ya udhibiti wa mataifa yoyote ya sasa na litakuwa katika mzingo wa dunia, eneo ambalo vyombo vya anga za juu huzunguka dunia.

Wanasayansi hao wanapanga kurusha satelaiti ya kwanza, ya kuanzisha taifa hilo, mwishoni mwa mwaka ujao.

Matumaini ya wataalamu hao ni kwamba siku moja hivi karibuni watatambuliwa na Umoja wa Mataifa.

Lakini baadhi ya wataalamu wanatilia shaka uwezekano wa mpango huo kufanikiwa ikizingatiwa kwamba sheria za kimataifa huzuia mataifa kudai umiliki wa maeneo anga za juu.

"Raia" wa Asgardia, ambao watachunguzwa kwa makini kabla ya kukubaliwa, mwishowe watapewa hata pasipoti, anasema Lena de Winne, mmoja wa maafisa wakuu wa mradi huo ambaye alifanya kazi kwa miaka 15 katika Shirika la Anga za Juu la Ulaya (EPA).

Maelfu ya watu tayari wameonyesha nia ya kutaka kujiunga na taifa hilo

Mradi huo unaongozwa na shirika la Aerospace International Research Center, ambalo lilianzishwa na mwanasayansi Mrusi, ambaye pia ni mfanyabiashara, Dkt Igor Ashurbeiyli.

Mashindano yanaandaliwa kuamua bendera na wimbo wa taifa wa nchi hiyo mpya.

Profesa Sa'id Mosteshar, mkurugenzi wa Taasisi ya Sera na Sheria za Anga za Juu ya London, amesema itakuwa vigumu kwa Asgardia kutambuliwa kama taifa ikizingatiwa kwamba haitahusiana na taifa lolote linalojitawala duniani, na pia 'raia wake' wengi watakuwa ardhini.

Tayari zaidi ya watu 50,000 wamewasilisha maombi mtandaoni kutaka kuwa raia wa taifa hilo!

Sunday, 16 October 2016

Zijue hatua 10 za kumpata mchumba sahihi.

Wengi wamejikuta wakiitwa wahuni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na makundi ya wanaume au wanawake. Hata hivyo wachunguzi wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni.

Watalaam hao wanataja safari ya kupata chaguo halisi la mwanaume/mwanamke wa maisha ndiyo inayowaponza wengi kiasi cha kujikuta wameingia katika kashfa ya kuwa na uhusiano na dazeni ya wapenzi.

Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya ngono, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake.

Kwa mantiki hiyo, bila upembuzi wa kina, mtu asiye na elimu ya jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli hujikuta ameangukia kwa mwanaume/mwanamke asiyemfaa, ambapo baadaye huamua kuachana na huyo na kwenda kwa mwingine kujaribu bahati tena ya kupata penzi la kweli.

Zinatajwa zawadi, hitaji la kusaidiwa kimaisha, mvuto wa kimahaba na mazoea kuwa ni vichocheo vinavyowaangusha wengi kwenye mapenzi na wasiowafaa.

Ukweli ni kwamba mtu aliyenaswa kwa ‘ujinga’, huwa hakatwi kiu ya penzi na mwanaume/mwanamke asiye chaguo sahihi la maisha yake. Hivyo hufikia maamuzi ya kujiingiza katika uhusiano mpya mara 2,3,4,5 na kujikuta wakiambulia wanaume/wanawake wale wale wasio sahihi kwake.

Mwanamnke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Ruth aliwahi kuniomba ushauri, akasema amechoka kuchezewa, maana kila mwanaume anayempata anakuwa si chaguo lake. Lakini kibaya zaidi kuachia ngazi au kutemwa huku akiwa tayari ameshafanya mapenzi na wanaume hao.

Nia ya swali lake ilikuwa ni kuniomba njia za kumtambua mwanaume mkweli bila kufanya naye mapenzi? Aliuliza hivyo huku akiwa na hoja kuwa wanaume wengi hawako tayari kuwa na uhusiano na msichana bila kufanya naye mapenzi na wakati huo huo huficha tabia zao chafu wakilenga kumnasa wamtakaye.

Binafsi nafahamu kuwa kuna wanawake/wanawake wengi ambao hujiingiza katika mapenzi kwa kutekwa na hadaa za mwili na kujikuta wanacheza mchezo wa kitoto wa pata potea.

Ni madhumuni ya somo hili kufundisha vigezo vya kumpata mwanaume/mwanamke halisi wa maisha, bila kufanya naye mapenzi. Njia hii ina faida kwa pande zote mbili yaani kwa mwanamke na mwanaume kwani kuacha au kuachwa bila kufanya mapenzi ni bora kuliko kuwa muonjaji, tabia ambayo huathiri kisaikolojia na ni hatari kwa afya.

Ifuatavyo ni njia ya kisaikolojia ambayo mwanamke anaweza kutumia kumpata mwanaume mwenye kumfaa bila kufanya naye mapenzi tena ni jibu sahihi la kuondokana na mchezo wa kubahatisha kwa wanaume wanaosaka wapenzi wa kweli na si taksi bubu ambazo mchana huweka namba za njano usiku nyeusi.

KWANZA- Ni ya mwanamke/mwanaume mwenyewe kujifahamu na kufahamu vigezo vya mpenzi anayemhitaji katika maisha yake. Ifahamike kuwa kila mwanaume ana wake na kila mwanamke anaye wake wa maisha pia. Hivyo asiyekufaa wewe anawafaa wengine, kinachotakiwa ni wewe kujitambua kwanza ili umtambue umtakaye.

Wanawake/wanaume wengi hawafahamu wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia kwa matapeli wa mapenzi, wakachezewe na kuumizwa moyo bure.

PILI- Ni kuketi chini na kuorodhesha vigezo stahili vya mwanaume/mwanamke unayemtaka. Baada ya hapo orodhesha tena kasoro za mwanaume/mwanamke unazoweza kuzivumilia na zile ambazo huwezi kuzivumilia kabisa. Hii inatokana na ukweli kwamba mwanadamu hajakamilika, ana upungufu wake.

TATU- Anza kumsaka kwa kutumia milango ya fahamu. Cha kufanya hapa ni kuruhusu macho yawaone wanaume/wanawake na kuwatathmini kwa maumbile yao ya nje na kisha kupata majibu kutoka moyoni juu ya kuvutia kwao ambako hutambulika kwa moyo kurithika na mwili kusisimka.

NNE - Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo. Hapa suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya kimapenzi na ngono. Kutambuana, dini, viwango vya elimu, kabila na makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.

Katika uchunguzi huu mwanamke/mwanaume anayetafuta mpenzi hana budi kupitia na kumlinganisha huyo aliyempata na vigezo alivyojiwekea. Zoezi hili liendane na kuweka alama ya pata kila anapobaini kuwa mwanaume/mwanamke anayemchunguza amepata moja ya vigezo vyake. Lakini pia aweke alama ya kosa kwa kila kasoro anayoivumilia na ile asiyoivumilia.

TANO - Ajipe muda wa kutosha kati ya miezi sita na mwaka kumchunguza huyo mwanaume, kisha aketi chini na aanze kujumlisha alama za vigezo alivyovijiwekea na jinsi mwanaume huyo alivyopata au kukosa.

Ikibainika mwanaume aliyechaguliwa amepata zaidi ya nusu ya alama ya vigezo vilivyowekwa, basi ujue kuwa anafaa. Kuhusu alama chache alizikosa anaweza kusaidia kuzikamilisha polepole wakati wa maisha ya ndoa.

Lakini angalizo kubwa kabisa ni kwamba mwanaume/mwanamke akionekana kuanguka katika kasoro zisizoweza kuvumilia kwa zaidi ya alama tatu. Yaani kwa mfano ni mlevi, mwizi, muongo, mbishi na katika hizo kashindwa 3, huyu hafai, ni vema akawekwa kando kwani huwezi kubeba kero 3 kwa pamoja katika maisha.

SITA - Kusajili mapenzi yenye malengo yanayotekelezeka. Lazima baada ya kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao. Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na wanapokwenda.

Hata hivyo watalaam wanasema lazima wapenzi wapime umakini wao kwa vitendo. Kama wamekubaliana kuoana, suala la mume kwenda kujitambulisha kwa wakwe na hatua ya kuiendea ndoa ionekane. Usiri usiwepo tena. Kila mmoja amuone mwenzake kama sehemu ya maisha yake na mara zote wasaidiane kwa ukaribu.

SABA - Ni vema ndugu wakashirikishwa ili kuwapa nafasi na wao ya kuamua kama mapenzi hayo ni budi yakaendelea au yakasitishwa. Ni ukweli ulio wazi kwamba licha ya wengi kupuuza maamuzi ya ndugu kwa madai ya kuwa hawana nafasi kwa wapenda nao, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi wengi huacha kutokana na sumu za ndugu hasa pale wanapokuwa wameonesha kutounga mkono uhusiano wa wanaotaka kuoana

NANE - Hatua hii ni ya kuweza kuzungumzia ufanyaji mapenzi, hapa nina maana kama wapenzi wamejizuia kwa muda mrefu na wanahisi kuchoka wanaweza kujadiliana kuhusu hilo na kuamua ufanyaji huo wa mapenzi una lengo gani, kama ni kuburudisha miili basi suala la afya na uzazi salama litazamwe.

TISA - Kutimizwa kwa ahadi ya kuoana ni hatua ya tisa ambayo nayo si busara ikachukua muda mwingi kutekelezeka, kwani ucheleweshaji mwingi wa ndoa nao huvunja moyo na mara nyingine umewafanya wengi kutoaminiana.

KUMI - Kuamua kuwa mwili mmoja kwa kuvumilia na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zote za maisha ukiwemo mkwamo na dhiki ambazo huchangia sana ndoa nyingi kuvunjika. Hapa pia ni wajibu wa wanandoa kuchukuliana udhaifu na kusaidia, kuwa tayari kujifunza na kujali zaidi upendo kuliko hisia za mwili ambazo wakati mwingine hudanganya na hivyo kumfanya mwanandoa asivutiwe na mwenzake.

Mwisho ni kwamba kanuni hizi huwafaa watu wazima mapenzi ya kitoto hayawezi kujenga misingi hii imara mara nyingi ni kudanganyana, kuharibiana maisha, kupeana mimba na maradhi.

NB: Kumbuka kumuomba MUNGU akupe chaguo sahihi. Ameen!

Utata mtihani wa Taifa wa darasa la pili.

MKANGANYIKO umeibuka kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwa mtihani wa taifa wa darasa la pili.

Wakati wapo baadhi ya wazazi wanaosema wamejulishwa kuwepo kwa mtihani huo, wengine wanasema wamepokea barua kutoka katika shule wanazosoma watoto wao kuhusu kuahirishwa kwake.

Hata hivyo, alipozungumza na gazeti hili hivi karibuni, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako alisema mtihani huo haupo kabisa.

Utata huo umeibua mkanganyiko kwa wazazi wengi, ambao watoto wao wanasoma katika shule mbalimbali za msingi nchini kutokana na kuwepo kwa shule ambazo uongozi wake, ulishatoa taarifa kwa wazazi juu ya kuwepo kwa mtihani huo, unaotolewa ili kupima uwezo wa wanafunzi kwenye KKK yaani Kusoma, Kuandika na Kuhesabu.

Wakizungumza na gazeti hilo kwa nyakati tofauti Dar es Salaam, baadhi ya wazazi walisema wamepokea barua inayowaeleza uwepo wa mtihani huo wa taifa, utakaofanyika Novemba 17 na 18, mwaka huu kwa lengo la kupima uelewa wa KKK.

“Nina barua nyumbani tulipewa shuleni kwa mwanangu anasoma Atlas School, barua inazungumzia mambo mengi pamoja na hilo la mtihani wa taifa wa darasa la pili na kwamba katika kutimiza hilo, wanafunzi wamepewa mtihani wa majaribio na wameufanya Oktoba 11 hadi 13, mwaka huu,” alisema mzazi mmoja.

Alisema mwanawe huyo anayesoma darasa la pili, hivi sasa anajiandaa na mtihani huo na wazazi wanafahamu kuwa mtihani huo upo kwa sababu walitangaziwa na shule.

Alisema, hata hivyo, hivi sasa wanafunzi wa darasa la kwanza na pili shuleni hapo, wanasoma masomo saba ambayo ni Kiswahili, Kuandika, Kusoma, Kuhesabu, Sayansi, Stadi za Kazi, Haiba na Michezo, hatua inayozidisha mkanganyiko.

Wakati mzazi huyo akisema hayo, mzazi mwingine ambaye mtoto wake anasoma darasa la pili katika Shule ya Msingi Tusiime, alisema awali wazazi walitaarifiwa kuhusu uwepo wa mtihani huo; na wanafunzi walianza kujaza fomu, lakini baadaye waliambiwa haupo.

‘’Nakumbuka shuleni kwa mwanangu waliambiwa kuhusu mtihani huo wa darasa la pili, na walianza kujaza fomu, ila baadaye wakaambiwa haupo, hatujui utafanywa lini,” alisema.

Mzazi mwingine ambaye mtoto wake anasoma Shule ya Mountain Hill jijini Dar es Salaam, alisema katika kikao cha wazazi cha Septemba, mwaka huu wazazi waliambiwa kuwa mtihani huo wa taifa kwa darasa la pili, umeahirishwa hadi mwakani.

“Nilienda kwenye kikao cha wazazi cha Septemba shuleni Mountain Hill na mwanangu anasoma darasa la pili, tuliambiwa mtihani wa darasa la pili wa taifa wa KKK haupo, bali utafanywa mwakani,” alisema.

Hata hivyo, Waziri Ndalichako alisema serikali haijawahi kuwa na mtihani wa darasa la pili; na kwamba watoto hao bado ni wadogo, hivyo hawastahili kupewa mtihani.

“Mtihani wa darasa la pili hatujawahi kuwa nao, halafu hawa watoto wadogo unaanza kuwapa mtihani, ni wadogo,” alisema Profesa Ndalichako, hatua ambayo inazidisha sintofahamu kwa suala hilo.

Thursday, 6 October 2016

Kagera tenaa, moto wawaka ardhini km volcano!


Wakazi Kagera wataharuki moto ardhini wakidhani volcano, wataalam watoa ufafanuzi!!!

Ikiwa zimepita wiki kadhaa tangu tetemeko la ardhi litokee Kagera, leo October 6 2016 kupitia kituo cha runinga cha ITV kimeripoti habari kutokea hukohuko Kagera ambapo wananchi wa bonde la Katarabuga wamepatwa na taharuki baada ya kuibuka moto ardhini wakidhani volcano. Wakala wa jiolojia, Prof Mruma amesema moto huo ni wa kawaida tu hivyo wananchi wasiwe na taharuki yoyote, Prof. Mruma amesema…….

Huu moto unaunguza ardhi ambayo umejaa vipandevipande vya miti mikavu majani, mizizi mithili ya mtu anayetengeneza mkaa’

Volcano haiwezekani hapa, volcano ni uji wa miamba na ya chini kabisa ya volcano degree 400 kwa hiyo degree 400 centigrade ikiungua hapa hata huu mti usingesalia, volcano mara nyingi inatoka na majimaji na mvuke’

huu ni moto wa kawaida, moto kama huu unatokea kwenye ardhi ambayo ina uozo wa majani mengi sasa yale majani yakiungua yanatoa kitu kama hiki, moto wa namna hii mara nyingi inatokea kwenye makaa ya mawe mtu anapita anaangusha moto mkaa unalipuka panaanza kuungua na ardhi inachubuka chubuka hivihivi!

Sunday, 2 October 2016

Je umekuwa addicted na simu yako? Jizuie na uraibu huo!

Jinsi Ya Kujizuia Na Uraibu (Addiction) Wa Kutumia Simu Janja Kila Mara!

Tafiti nyingi zimefanyika na ukweli umegundulika ni kwamba wengi wetu tumepata na uraibu (addiction) juu ya smartphone zetu pengine kuliko vitu vingine.

Kumbuka kuna wengine wanazipenda sana simu zao na hata zikidondoka wao ndio huumia Hahaha! .
Kwa karne hii wengi wanatumia simu janja (smart phone) sana kuliko zile simu zingine (mwanga wa sabuni).

Ukaribu wao wa kupitiliza na simu hizo pengine ndio unaosababisha uraibu (addiction) huo.
Katika tafiti iliyofanyika huko British, ilidai ya kwamba katika kila watu watatu (3) basi lazima kuna mmoja ambaye lazima atakuwa anatumia simu yake usiku wa manane.
Sasa kama ukijihisi una uraibu na simu yako nini cha kufanya? Njia ni hii hapa.

1. Weka Simu Yako Mbali Na Ulipo
Ndio! kama simu iko mbali na wewe ulipo hutaweza kuitumia sio? Kuna wengine hapa bado ni changamoto kwani hawawezi kukaa mbali kabisa na simu zao. Lakini kuna wale waliobarikiwa (Kama rafiki yangu, Mmaryson ) wao wanaweza hata kusahau kabisa walipoweka simu zao mpaka atokee mtu abipu hiyo simu.

2. Futa Baadhi Ya App
Kama unasumbuliwa na uraibu wa simu basi hapo huna budi kufuta baadhi ya App. Na itakua ni vizuri kufuta zile unazozipenda kwani hamu ya kushika simu na kuzifungua mara kwa mara itapungua au itaisha kabisa. Kwa kifupi ni kwamba utashindwa kushika shika simu yako kila mara.

3. Zima Simu Janja Yako
Hivi mara yako ya mwisho kuzima simu yako ni lini? Kuna wengine wanachanganyikiwa kabisa kama simu zao zikizima. Unaweza ukajiwekea katabia ka kuzima simu yako, pengine labda ukiwa bize au ukiwa unalala. Hii kwa kiasi kikubwa itapunguza uraibu kwani hutapoteza muda kupepesa machi katia simu yako hiyo.

4. Jiwekee Muda Maalamu Wa Kutotumia Simu Yako
Wengine wanajiuliza Je, ni kweli inawezekana? Lakini mimi naamini kila kitu kinawezekana. Ukijiwekea muda maalumu ambao hutaweza kugusa simu kabisa itakua ni vizuri na uraibu utapungua kwa kiasi kikubwa. Kwa mfano unaweza ukajiwekea katabia kwamba kila ifikapo saa mbili usiku hutakua unatumia simu mpaka kesho yake.

5. Usitumie Simu Yako Ndani Ya Dk 30 Za Kwanza Baaya Ya Kuamka.
Ukishaamka asubuhi usifanye kuangalia simu yako kuwa ndio kitu cha kwanza kufanya. Fanya vingine vya muhimu unaweza fanya mazoezi pia na ukafanya maandalizi ya kuweza kupata chai. Haya yote yakitumia ndipo unapoweza rudi katika simu janja yako na kujua yale yaliyojiri.
Kama inavyofahamika kuwa uraibu wa aina yoyote ile una kazi sana kama mtu akitaka kuacha hicho kitu ambacho ana uraibu nacho. Hapa cha msingi ni juhudi na dhamira ndiyo itakayo saidia. Kwa Tanzania pengine jambo hili linaweza likachukuliwa Poa!

Lakini nina uhakika wapo watu amabao wanasumbuliwa na hili, ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini kama kuna njia yeyote ambayo sijaiandika na unahisi inaweza pia ikasaidia.


Saturday, 1 October 2016

Ongeza nafasi ktk disk yako!

Jinsi ya Kupata Nafasi ktk ‘Hard Disk’ Iliyojaa

Umejaza filamu na nyimbo kibao katika diski yako, labda ni magemu pia. Tamthilia je? Inaweza ikawa moja ya vitu hivi au ni mambo mengine kibao yamejaa kwenye kompyuta yako kiasi ya kwamba inakuwa ni vigumu ata pa kujua mafaili makubwa ya kufuta ni yapi hasa.

Unaangalia kompyuta yako na inakuambia diski C yako inakaribia kujaa kabisa na hivyo unatakiwa ufute baadhi ya mafaili, ila ndio hivyo tena kutokana na jinsi yalivyomengi hufahamu mafaili yapi ni makubwa au yapo wapi hayo makubwa kutokana na wewe kuwa na mafolda mengi kwelikweli. 

Leo tunakutambulisha kwa programu moja ya bure kwa watumiaji wa kompyuta/laptop za Windows, inaitwa WinDirStat.
Ndio kuna njia zingine za kupunguza nafasi katika diski yako kama vile kutumia programu wa Windows ifahamikayo kama ‘Disk Cleaner’, ila hiyo haikuoneshi mafaili yako mwenyewe. Yenyewe inasaidia mafaili ya system ya kompyuta tuu.

Programu ya WinDirStat inakupa uwezo wa kufahamu mafaili gani ni makubwa na ni kwa ukubwa gani na pia inakupa uwezo wa kuyafuta kwenda kwenye ‘Recycle Bin’ au kuyafuta moja kwa moja kabisa bila kupitia Recycle Bin.


Pia kwa kutumia rangi mbalimbali utaoneshwa mafaili muhimu ambayo si vizuri uyaguse ukapoteza vitu vya msingi!

Linda data zako kwa njia hizi 5 uwe salama!!!

Njia Tano za Kulinda Data Zako Sasa

Je, wewe ni moja wa watu walio na msukumo mkubwa wa kulinda data na maisha yako ya kidijitali? Hii inakuhusu sana.
Mara nyingi tunasikia ya kwamba mitandao mbalimbali na huduma za mtandaoni zinavamiwa na wahalifu wa mitandao na katika nyakati hizo mtu wa kawaida hauna mengi unayoweza kuyafanya kukabiliana na matatizo kama hayo. Watu husema kinga ni bora kuliko kutibu yaliyojiri, hivyo kuna vitu rahisi unavyoweza kufanya kabla ya majanga ili kujilinda na uhalifu wa mitandao kama:

1. Ruhusu Roboti Kumudu Pasiwedi Yako
Kwa kawaida, akili ya binadamu haina uwezo mkubwa wa kukumbuka pasiwedi na hata kutengeneza nzuri, yenye ugumu wa kudhibiti kuvamiwa.
Mara nyingi tunatumia pasiwedi ileile kwenye tovuti mbalimbali. Hili sio jambo zuri. Linamaanisha kwamba kama mhalifu akigundua na kuvamia akaunti mojawapo unayomiliki, anaweza kuingia kwenye akaunti zako zingine.
Hili ni tatizo kubwa hasa ukizingatia watu wengi wanasemekana kufanya hivyo kwenye akaunti zao za Facebook, Google, Twitter na hata akaunti za benki za mtandaoni.
Suluhisho la jambo hili ni kutumia huduma moja ya kumudu pasiwedi zako za kompyuta na simu ambayo itaipa kila tovuti uliojisajili passiwedi isiyo na mpangilio maalumu mara kwa mara na kui-’synchronise’ kwa vitumi vyako vyote. Mifano ya huduma kama hii na ambayo inajulikana sana ni kama 1Password na LastPass.

2. Pata U2F – na Tumia Uidhinisho wa Aina Mbili
Njia nyingine ya kulinda akaunti zako ni kuhakikisha kwamba hata kama mtu ataijua passiwedi yako, hatakuwa na idhini ya kuingia kwenye akaunti hiyo moja-kwa-moja.
Ili kuingia kwenye akaunti, inabidi awe na uidhinisho wa ziada, yani tofauti na pasiwedi. Kwenye baadhi ya tovuti, hii inaweza kuwa namba ya siri inayotumwa kwenye simu yako kutoka kwa tovuti/ huduma husika (kama unavyotumiwa na WhatsApp unapo-’sign-in’), au kuanzisha app maalumu ya ziada kwenye kifaa chako ambayo itatoa namba ya siri ya kutumika mara moja.
Moja ya njia mpya kabisa kama hizi za uidhinisho wa mara mbili ni ‘U2F security key’, ambayo ni kwa kutumia kitu kinachoonekana kama flashi ya USB ya kawaida. Bila ya kifaa hicho, huwezi kuingia kwenye akaunti flani kwenye kompyuta yoyote. Kifaa kama hiki kinaweza kugharimu kama dola 15 za kimarekani (TShs 30000) ambayo ni gharama ndogo ya kukuongezea usalama wa data zako. Tayari ishaonekana kwamba ndani ya miaka michache inayokuja, makampuni makubwa yataongeza matumizi ya U2F.

3. Wezesha ‘Disk Encryption’
Kama una laptopu au simu ya mkononi ambayo haijawezeshwa na ‘Data Encryption’ na ikaipotea, ujue kwamba mtu yeyote ambae ataipata ana uwezo wa kupata data zako kirahisi.
Data Encryption ni mbinu maalumu ya kuficha data zako kwenye kifaa kwa kuzipa data hizo mfumo usiosomeka iwapo mtu akiamua kuflash hicho kifaa na kujaribu kuibua data zako. Mbinu hiyo imewekwa moja kwa moja kwenye i-phone na iPad ila kwa Windows, Android na Mac OS inabidi utumie muda wako kidogo ili kuiwezesha. Jambo hili ni la msingi kwa wale walio na ‘unyeti’ wa data zao na maisha yao ya kidijitali.

4. Weka Stika kwenye Kamera ya Kompyuta
Imejulikana kwa muda mrefu kwamba kuna watu mtandaoni wana tabia ya kuwasha kamera zilizopo kwenye laptopu zisizo za kwao kwa makusudi ya kuchungulia kila unachofanya bila wewe kujua. Hiki kitu hakitokei mara milioni kwa mwaka ila bado kinatokea ni kitu kinachotokea mara kwa mara na cha kutisha. Unaweza kujilinda na wahalifu hawa kwa kuweka stika kwenye hiyo kamera uwapo huitumii.
Unaweza kujilida na wahalifu kwa kuweka stika kwenye hiyo kamera uwapo huitumii.

5. Encrypt Mawasiliano yako ya Simu na Ujumbe
Mawasiliano ya simu na meseji ambazo makampuni ya simu yanatoa yana uwezo wa kufuatiliwa na mtu yeyote mwenye nia . Hii ina maana kwamba serikali yako au ya nchi nyingine na watu wenye maslahi ya kuiba ujumbe na mazungumzo yako kwenye simu wanaweza kupata chochote wanachotaka bila ya nguvu nyingi. Baadhi ya app za intaneti kama WhatsApp na FaceTime zinaweza kuwa nzuri ila kama ungependa usiri zaidi, fanya tafiti kidogo kupata huduma zenye usalama wa hali ya juu kama Signal inayopatikana kwenye Apple Store.


 

Sunday, 25 September 2016

Jiepushe na dark website hatari!

Simu au Computer yako ina hizi tabia?
1. Kukuletea matangazo ya Kudownloada vitu usivyovijua?
2. kupokea emails nyingi za watu wanaomba account yako wakutumie hela?
3. kuletewa matangazo bila mpangilio wakati upo mtandaoni?
4. Kujiconnect kwenye website bila taarifa?Kama unatatizo hata moja hapo, basi wewe ni muhanga wa hiki kitu ninachokieleza hapa chini;

Hii ni elimu muhimu kwako sababu itakuongezea usalama ktk mambo yako ya muhimu na siri zako unazotunza ktk mitandao kwa kutumia SIMU au COMPUTER yako.

Duniani kuna website za aina nyingi sana na zinafanya kazi kwa mifumo tofauti, na baadhi yetu hupenda kusafu mitandaoni kila siku kwa kutembelea website nyingi na kwa wingi.

Website hizo zinamilikiwa na watu tofauti na zipo kwa malengo tofauti na pia zinafanya kazi kwa mifumo tofauti, Leo nitaongelea Website za aina fulani inayojulikana kwa jina la “Dark websites” yaani website giza au website nyeusi.

Sasa basi ninaomba niende moja kwa moja hapa kwenye mfumo unaotumika ktk hizi Dark Websites wakati wa utanyaji kazi; mara nyingi huwa zinaomba ujaze vitu vifuatavyo kabla haujaendelea na chochote; 1. Jina lako2. Email yako 3. Password zako Mfano mzuri ni kama (facebook, sasa basi naomba nieleweke kuwa kuna “Dark Website SALAMA” na pia kuna “Dark WebsiteHATARI“)

Licha ya kuwa Facebook ni aina ya “Dark website salama” lakini kuna watu walikwisha tengeneza website zinazofanana na facebook kwa kila kitu na hizo tunaziita “Dark websiteHATARI“Huo ni mfano mmoja tu, LAKINI zipo website za namna hiyo nyingi sana (Itafika siku nitakuonyesha ni namna gani Hackers huingilia Account za watu za Facebook)

Kwa leo ninaomba tuendelee na hiki kitu ;“Dark websites HATARI” hufanya kazi kama Dark website salama, na hizo Darkwebsite hatari nazo huwa zinaomba ujaze vitu kama jina, email, password ili uweze kupata unachohitaji, lakini wengi wetu hatufahamu madhara yake, Leo nitakwambia kwa ufupi sana kuhusu wale watu Wanaoingilia account za watuwengi bila wahusika kufahamu hutumia mbinu gani,Wao huleta kitangazo kizuri sana tena kina picha nzuri nzuri zikikwambia “download” au “open” au “get this” na wewe kweli masikini bila kujielewa unabonyeza!

Ukifanya hivuo unapelekwa sehemu hatari bila kufahamu, na ukiingia huko utakuta kuna sehemu zinakutaka ujisajili, na wengi wetu huwa tunajaza tu data zetu bila kuelewa tunapelekwa/zinapelekwa wapi.

Nikupe siri sasa, “Dark websites HATARI” ni website feki zinazotumiwa na wahalifu kukusanya data au taarifa za watu, na mara nyingi kwa wale wanaopenda kudownload vitu wasivyovijua. Ukiwa ndani ya Dark website hatari wala hautagundua chochote hadi uwe na software/antivirus ya kukujulisha kuwa upo hatarini!

Mara nyingi ukiwa humo huwa kuna mdudu anaitwa “Malware” anajidownload bila wewe kufahamu na anaingia ktk simu au Computer na anajificha.Kazi yake kubwa ya huyu mdudu ni kuiba data zako muhimu na kuzituma kwa mmiliki wa hiyo Dark website Hatari, (Wataalamu wa IT wengi huwa wanaweza kuziset hizi Dark website HATARI hivyo ninaamini wananielewa vizuri)

Namna ya kuepuka; Njia ya kwanza; Ukiwa na simu au Computer unaweza kutumia Antivirus inayoitwa Eset Node 32 Antivirus ambayo ina protection nyingi zikiwemo hizo za kuzuia Dark websites HATARI, kwa wenye simu mtaipata play store kwa kuandika neno “eset” na kubonyeza search/go, itatokea ya kwanza kabisa imeandikwa “Mobile Security & Antivirus”

Na wenye Computer mtaipata hapa ⇒  https://maxitclub.wordpress.com/antivirus-nzuri/mimi binafsi huu ni mwaka wangu wa 3 ninaitumia na nipo salama), kwa wenye Computer ninawashauri muachane na kutumia Antivirus nyingine hizo zinazo wasumbua ku update kila siku.

Njia ya pili; Epuka kupokea simu, sms na email zinazotoka sehemu zisizo julikana “Unknown sources” nafahamu wenye Smartphones mnajua hiki kitu, kuwa kuna sehemu imeandikwa “Allow installations from unknown sources”, hawa jamaa wanafahamu kila kitu na ndio maana wamekuachia jukumu ujiamulie mwenyewe.

Njia ya tatu; Epuka kudownload au kubonyeza hovyo matangazo usiyokuwa na taarifa nayo, na mara nyingi huwa yanakuwa ni matangazo ya Ngono, Miziki, Biashara n.k, acha hiyo tabia ya kubonyeza kila uachokiona.Hitimisho;Hasara ya kuingia kwenye Dark Website HATARI, utakuwa unaona text au email zinaingia kila siku na nyingi huwa zinakuja na majina ya kike zikiomba ujibu na pengine mtumiane picha, au nyingine zikikudanganya kuwa kuna hela zipo sehemu hivyo basi usaidie kwakutuma account namba yako ya benki ilizihamishiwe kwako.

Walio wengi huwa wanafanya hivyo, lakini hatari yake ni kubwa, ipo siku utafanyiwa kitu kinaitwa“HACKING” kwa kiswahili ni “KUINGILIWA KWENYE ACCOUNT ZAKO BILA KUFAHAMU“ Ushauri; kwa wafanyakazi mnaofanya kazi kwenye makampuni makubwa kama yanayojihusisha na mambo ya Fedha, Usalama, Huduma za Afya, Wahasibu Vyuoni au Mashuleni, Viongozi wakubwana wadogo Au watoa huduma zozote za muhimu ktk jamii mnatakiwa muache kabisa tabia ya kujaza hovyo data zenu mahala msikokujua.

Aidha kwa wasio wafanyakazi pia mnapaswa kuacha ili kuwa salama zaidi.

Wednesday, 21 September 2016

After work, is what determines your Life! Change ur Life forever by doing this 5 things!

Kalyana SundaramBusiness Development Manager - SAP

After work, is what determines your future! Spend one hour per day doing these 5 things and your life will change forever!

May 19, 2016 • 35213 Likes • 2726 Comments

You finish work at 6 pm, go to bed at 12 midnight.

Within these six hours, how do you spend them?

Watching TV?

In fact, the activities you do between 6 am and 12 midnight,

the importance of it is beyond your imagination.

Too many people believe that,

your career is determined by the 8 hours of hard work and effort you put at work,

and your future and career progression depend on the boss and the company.

But the reality is that for most people, this thing, you are on your own…..

 

Read on…

 

“Cultivation”, it’s forever dependent by yourself.

If you found yourself not progressing in life,

you cannot blame and put the responsibility on your company for not grooming you.

 

1. What you do every night is important

My major in college was marketing, but I expect to become a designer.

So I practiced day and night,

picking up some freelance work to improve my design skills.

It took me a long time.

When I became a boss, I no longer need to involve myself in design work,

So I went back to the Marketing field.

Every day, when my children are sleeping,

I began learning to gain more knowledge, this again took me a long time,

But I begin to realise my returns.

 

If I rely on my working hours to gain skills,

then I will never have become a creative director and a product manager,

or like today, teaching MBA students on Marketing.

What I rely on, is myself giving myself “lessons”.

And the most successful people I knew, walked the same path as I am.

I have a friend who is a History graduate,

but he is interested in technical sales,

In the day, he does telemarketing, at night he learns how to code,

Finally, he became the vice president of sales in a startup company.

Now, he’s a CTO.

I have another friend, he received a degree in political science.

But he’s very interested in entrepreneurship.

he learnt a lot of knowledge on how to start up a company,

eventually, he founded a company and sold it,

Now he has reaped the rewards.

 

For them, what they do between 6 pm till 12 midnight,

is what determined their future.

Clearly, we need to balance life and work.

If you have a wife and children, every night, you have to stay with them.

Even if you are single, you also need a reasonable allocation of time to go to the gym, to meet with friends, or be alone to meditate and so on.

Of course, watching movies, playing games is good.

But there are things you do not need to do.

For example, watching the new season of a Netflix drama,

14 hours per week watching television (This is the average amount of time watching television).

 

The time spent playing the game Candy Crush.

 

Or spending time stalking your high school alumni on Facebook,

it does not seem to be good.

So what should you do?

 

2. Read more, anything will do!

My college mentor was born in Alabama,

A poor African family.

He was admitted to West Point Military Academy, and he became the first person in the family to go college.

Before going to Havard for his MBA, he’s a trained officer.

When I met him, he has already developed his career in the city of Colorado Springs.

 

I asked him, what’s his biggest success?

He replied, because he kept the habit of reading,

and he never stopped.

He believed that if you want to get what you want in life,

knowledge is the key.

He often asked his interviewees what book are they reading now,

the excellent ones can give an answer immediately.

Reading can give you a good headstart,

this is often what your peers cannot obtain.

Compared to others,

you are more likely to know other industries strategies and tactics,

and that may be helpful to your company.

 

You can transfer your knowledge within the organization,

create new possibilities for your company.

Moreover, your conversation topics will become more interesting.

 

Anthony Robbins said:

“If you spend one hour a day to learn about a topic,

a year later, in this regard,

the knowledge you gain will be more than 99.999% of the world’s people.”

Even if you have 30 minutes every night,

each week you can easily read a book.

You may not be an expert, but I promise,

you’ll know more than what your peers know.

 

3. Do some projects

You can apply the knowledge learnt to real work scenario,

this is only an ideal state.

If your company did not give you this opportunity,

create opportunities for yourself.

You can do some volunteer projects. They can bring you fame.

Working with a team,

you’ll understand how things work.

In the practical application of the industry,

and how it ultimately affect actual customers.

You’ll learn how to perform the task and meet deadlines,

and get feedbacks on what you are doing,

and benefit from it.

 

When you are not strong enough, these experience may not have any value to you.

But you are still a novice.

these experiences are far more valuable than the miserable pay you are getting.

If you can really convince others of your pockets of fruits of labour,

Then go try it. But do not let these private jobs affect your work.

 

4. Actively build your connections

In your career path,

a strong network of connections will make everything accelerate.

If you have not set up your own personal connections,

you’ll need to divide a portion of your time to do this.

A strong network of relationships, can enable you:

contact smart friends, and learn their opinionsget information and knowledge that are difficult to obtainhelp the company look for more potential partnersor income generating opportunities

Go get to know your work colleague or boss…..

 

If you are an entrepreneur,

your network connections will be your early customers,

your staffs are a source of capital

rather than go home, or going to a bar,

you should find some inner circles.

There are many small groups which are highly relevant to your career.

You should try to integrate into these circles.

Every week, you can drink coffee together with new friends,

go drinking or have breakfast.

 

You can also look into everyone’s career developments on LinkedIn.

And establish a network with mentors in those professional industries.

They may be your next job employer, who knows?

Your connections will be your most powerful asset in the workplace.

Since you have time to watch “The Voice of China”,

you have time to build a social network.

 

5. The CHANGE of your LIFE starts TONIGHT

6 pm to 12 am, you go home, though physically and mentally tired,

you are free to do anything and do not have to take orders from others.

During this time,

you can switch off like switching off your computer at your workplace, switch off your brain.

But you can also do something,

make you smarter, stronger, have a wider network of people.

From the start tonight, take an hour a day to do these things,

I guarantee that after a year,

your career, and life will change.


Tuesday, 20 September 2016

Mheshimiwa abambwa gesti na bintiye!

Mheshimiwa Abambwa Gesti na Mwanaye!

DAR ES SALAAM: CHAR/RB/1847/2016 KUJARIBU KUBAKA ni RB ya Kituo cha Polisi Mbagala Charambe jijini hapa  ikimhusu moja kwa moja mheshimiwa Damian Edward Kakuru, mkazi wa Mwandege wilayani Mkuranga, Pwani kufuatia askari wa kituo hicho na ‘makachero’ wa Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ kumnasa ndani ya chumba namba 6 kwenye gesti iliyopo Mbagala, Dar akiwa na binti yake (16), jina tunalihifadhi kwa sasa, Wikienda tu linakujuza zaidi.

SIKU YA TUKIO

Mheshimiwa Kakuru alikumbwa na tukio hilo zito katika kumbukumbu za maisha yake, Septemba 15, mwaka huu akiwa kwenye chumba hicho katika harakati ambazo ziliashiria ni za nia ya kutaka kujaribu kumbaka binti huyo ambaye kisheria yuko chini ya miaka ya kujitambua kwa maamuzi, 18.

KWA NINI MHESHIMIWA?

Licha ya yale yaliyotokea, mzee Kakuru inadaiwa amekuwa mzee wa Kanisa la Truth Ministry International lakini pia

 Inatoka Uk. 2 anaheshimika katika jamii ya maeneo anayoishi. Sehemu ya mavazi yake ni zile suti za viongozi huku wengine wanaoonekana kuzivaa sana ni watu wa usalama wa taifa hali inayomfanya asilikwepe jina la mheshimiwa kwa watu wa Mwandege.

MWANAYE KIVIPI?

Kabla ya kuendelea na tukio hilo, muhimu kufahamu ni kwamba, mzee Kakuru ana wake wanne. Mmoja wa wake zake, anayeishi mkoani, ana mdogo wake wa kike, ndiye mwenye mtoto huyo. Hivyo, alipofika kuishi kwa mzee huyo, maana yake yupo kwa baba yake mkubwa. Na maisha yao nyumbani hapo ni ya mtu na mtoto wake; ‘shikamoo baba, marahaba mwanangu’!

SASA TWENDWE PAMOJA

Jumba bovu hilo ‘lilimwangukia’ mzee huyo baada ya binti yake kulalamika mara kadhaa kwa watu anaowaamini kuwa, baba yake huyo amekuwa akimshawishi kutenda tukio ambalo yeye anaamini ni la ‘watu wazima’ na wasio na uhusiano wowote. “Binti amedai kuwa kutokana na mazingira hayo kudumu kwa muda mrefu, aliwahi kumshtakia kwa mama yake lakini ilionekana kama mtoto ana uelewa mdogo katika kupokea mambo na kuyatafsiri, lakini pia ilibidi kuwe na kikao cha kifamilia ili kumaliza madai hayo,” kilisema chanzo kimoja.

KIKAO CHASHINDWA KUFUA DAFU

Hata hivyo, kwa mujibu wa chanzo, licha ya kikao binti huyo alidai baba yake huyo aliendelea kumsumbua hali iliyomsukuma binti, safari hii kuhamishia malalamiko yake kwa walimu katika shule ya sekondari (jina lipo) ambapo binti huyo anasoma na sasa yupo kidato cha nne.

WALIMU WAPELEKEWA MALALAMIKO

Wikienda lilitajiwa orodha ya walimu ambao, binti huyo alifungua kinywa chake kuwatonya anachokutana nacho kwa baba yake huyo. Walimu hao walitajwa kuwa ni Mapunjo (jina moja, mwalimu mkuu), Adamu Nyema (mwalimu wa malezi), mwalimu Hokororo na mwalimu Said ambao binti huyo alidai wote wanafahamu malalamiko yake.

WALIMU NA MAMA MZAZI

Chanzo kikazidi kuweka wazi kuwa, baada ya kupokea malalamiko hayo, walimu hao waliwasiliana na mama wa binti aitwaye Goret Kabogwi ambaye anaishi Kamachumu wilayani Muleba, Kagera. “Lakini kinachoonekana ni kwamba, mawasiliano ya walimu na mzazi wa mtoto huyo hayakuzaa matunda kwa kuwa walimu walikuwa wakitaka kumchukua mwanafunzi huyo ili wakaishi naye mpaka atakapomaliza shule arudi kwa mama yake lakini taratibu za kisheria za kuishi na binti huyo zilionekana kuwa ngumu hivyo kumuacha njia panda.” Chanzo.

HADI KANISANI

Chanzo: “Wakiwa katika kutafuta nini cha kufanya, binti huyo aliendelea kutafuta ufumbuzi mwenyewe ambapo sasa alilipeleka suala hilo kanisani ambako ndiko alikotokea muumini mmoja aliyemuongoza binti huyo

kuwasiliana na OFM na kumhakikishia kwamba, suala lake litakuwa limekoma kama siyo kwisha kabisa! BINTI NA OFM Mungu si Kalimanzila, Septemba 14, mwaka huu, binti alifanikiwa kukutana na OFM uso kwa macho na kusema yote kuhusu mzee huyo huku akirekodiwa kwa sauti na picha kwa ajili ya kuboresha kazi.

USHAURI WA OFM

Baada ya maelezo yake hayo, OFM walimtaka binti huyo kama ni kweli, kufuata maelekezo kama siyo maagizo. Binti huyo alielekezwa na OFM kumkubalia baba yake huyo ili wanaswe wakiwa gesti, jambo ambalo litaongeza ukweli wa malalamiko yake. Binti: “Sawa, mimi nimewaelewa, lakini sasa nikirudi nyumbani, baba akaniambia tena maneno yake mimi nitawapataje ninyi? Maana sina simu!” OFM: “Sisi tutakupa simu na namba zetu zitakuwemo humo, sawa ee?” Binti: Sawa, nitashukuru sana. Maana nimekuwa sisomi nikaelewa, kisa ni

kusumbuliwa na baba.” OFM: “Usijali binti, yataisha hayo, OFM ni kazi yetu kuhakikisha maadili yanasimama sawasawa na inavyotakiwa.” BINTI NYUMBANI Baada ya kurudi nyumbani, kama kawaida, mzee huyo bila kujua kuwa, OFM wapo kazini, alimwambia binti yake yale maneno. Safari hii, binti alikubali kwa urahisi lakini akaomba eneo la tukio lisiwe nyumbani bali sehemu nyingine yoyote ili kutunza siri. Alipewa maelekezo kuwa, kesho yake, apande daladala kutoka Mwandege hadi Kituo cha Kokoto, Mbagala ambako atakutana na mzee huyo na kutafuta sehemu yenye utulivu kwa ajili ya ‘mazungumzo’ yao.

Binti akawasiliana na OFM, akaambiwa good!! SEPTEMBA 15, OFM POLISI Asubuhi ya siku ya tukio, binti huyo aliiambia OFM tayari baba yake ameshamuelekeza eneo la kukutana ambapo OFM nao wakaenda kumjulisha Mkuu wa Upelelezi Polisi Wilaya ya Mbagala (OC-CID), Tobias Walelo na kumueleza mpango mzima. Afande Walelo baada ya kusikiliza kwa umakini maelezo na kuambiwa OFM wanasubiri ushauri wake, alisema amegundua kuna kosa la jinai, aliwataka OFM kwenda Kituo cha Polisi Charambe ambapo ni karibu zaidi na eneo la tukio na kumtaarifu suala hilo mkuu wa kituo hicho.

OFM, ASKARI GESTI

Mipango ilisetiwa, maafande wa kituo hicho na OFM waliongozana kwenda gesti kwa maelekezo ya binti huyo kupitia simu ya mkononi ya OFM na kujibanza sehemu kwa siri. Baada ya dakika kadhaa, mzee Kakuru alionekana akiwasili eneo hilo akiwa amevaa suti iliyonyooshwa kwa pasi vizuri. Alimkaribia binti huyo na kumwonesha tabasamu laini kisha wakaanza kukata vichochoro, baba mbele binti nyuma. OFM na polisi wakiwafuata kwa nyuma kimtindo, wawili hao walimaliza vichochoro kadhaa kisha wakatokea kwenye  nyumba ya wageni iliyotulia, walizama ndani kwa pamoja.

POLISI KWA MHUDUMU

Polisi walisubiri kwa dakika chache kisha wakaenda kwa mhudumu wa gesti hiyo na kumtaka awaoneshe chumba walichoingia wawili hao. Kwa kutii amri ya jeshi la polisi, mhudumu huyo aliwaonesha chumba namba 6 ambacho alisema hadanganyi!

BINTI ALIVYOJIONGEZA

Kwa kuwa katika kuingia ndani ya chumba, binti huyo ndiyo alikuwa nyuma hivyo alitumia nafasi hiyo kuufunga mlango kwa geresha, kitendo kilichowasaidia polisi na OFM walipofika mlangoni kusukuma na kuingia ambapo wawili hao walikutwa nusu utupu!

BABU AJING’ATANG’ATA

Baada ya kunaswa laivu, baba huyo aliwatolea macho polisi na kuulizwa kwa nini yuko chumbani na binti huyo ambapo alisema alikuwa na binti yake kwa ajili ya kutatua tatizo fulani lililopo kati yao. “Hapa sisi tumekuja kusuluhisha mgogoro, ninyi mnataka nini? Hebu tuacheni.”

KWA NINI MGOGORO USULUHISHWE GESTI?

Mheshimiwa huyo alipoulizwa sababu ya kusuluhishia mgogoro gesti, awali alikaa kimya kisha akasisitiza walikuwa wakitaka kusuluhisha tatizo.

MASHUHUDA WATAKA SHERIA IFANYE KAZI

Mashuhuda wa tukio hilo waliozungumza na OFM waliitaka serikali kusimamia kikamilifu sheria iliyopitishwa kwa kishindo na wabunge mwezi Juni, mwaka huu ya kuwabana wale wote wanaotembea na wanafunzi  na watoto wa kike walio na umri chini ya miaka 18.

Friday, 16 September 2016

Je, huwa unakoroma? Je wajua sababu na jinsi ya kuzuia?

Sababu ya kukoroma na jinsi ya kuzuia hali hiyo!

Kukoroma ni tatizo linalowapata watu wengi wakati wanapolala ambalo linaweza kuwatokea watu wa kila umri ingawa hutokea mara nyingi kwa wanaume au watu wanene. Kukoroma huzidi kwa kadri umri unavyoongezeka na asilimia 54 ya watu wazima hukoroma baadhi ya wakati huku asilimia 25 ya wengine wakiwa na tabia ya kukoroma kila wakati. Kukoroma baadhi ya wakati kwa kawaida sio tatizo kubwa na mara nyingi huleta tu karaha kwa mtu anayelala karibu na mkoromaji.

Hata hivyo kukoroma huko sio tu kwamba huharibu usingizi wa anayekoroma bali pia huwasumbua na kuwakeresha wanaolala karibu na mkoromaji. Wale wenye tabia ya kukoroma, hukoroma kila wanapolala na mara nyingi huchoka wanapoamka, na watu wa aina hii hushauriwa kumuona daktari na kushauriwa kuhusiana na tatizo hilo. Lakini kabla hatujaendela mbele ni bora tujue kukoroma hasa ni nini au hutokea vipi?

Mtu huwa anakoroma pale kunapokuwa na kitu au sababu yoyote itakayoziba kuingia au kutoka kwa hewa mdomoni na katika pua. Kuta za koo hutikisika wakati wa kupumua na matokeo yake ni sauti inayosikika ya kukoroma. Kuingia au kutoka kwa hewa huweza kuzuiwa na sababu mbalimbali kama vile:

• Kuziba tundu za pua kusiko kamili ambako husababisha nguvu zaidi zitumike katika kupitisha hewa kwenye pua wakati mtu akiwa amelala. Kitendo hicho hupelekea nyama laini za pua na koo zijikusanye na kusababisha mkoromo. Kuna baadhi ya watu wanakoroma tu kipindi cha allergy (allergy season) au wanapatwa na matatizo ya sinus. Baadhi ya matatizo kama vile kupinda pua (deviated septum) au ukuta unaotenganisha tundu za pua na polyps za pua pia huweza kufanya pua zizibe na kusababisha kukoroma. Watu wengi wanaofanya operesheni za pua pia hupatwa na tatizo la kukoroma.

• Kuwa na misuli dhaifu katika koo na ulimi. Misuli au nyama za koo na ulimi zinapokuwa dhaifu sana hulegea na kuanguka upande wa nyuma wa sehemu inayopita hewa. Suala hilo hutokea pale mtu anapolala fofofo au kuwa na usingizi mzito na kusababisha kukoroma.

• Kuwa na misuli minene ya koo. Hii ni kwa wale watu wanene ambao hata nyama zao za koo pia hunenepa na kupanuka na suala hilo husababisha kukoroma, Pia watoto wenye tonsesi kubwa na adenoids baadhi ya wakati hukoroma.

• Kuwa na kilimi kikubwa ni mojawapo ya sababu zinazosababisha kukoroma. Kilimi kirefu kinaweza kuzuia koo na pale kinapotikisika wakati hewa inapita kwa msukumo husababisha kukoroma.

• Sababu nyinginezo zinazoweza kumsababishia mtu akorome anapolala ni kuwa na umri mkubwa au uzee, imeshuhudiwa kuwa watu wa makamo na wazee hukoroma, kwani misuli na nyama za koo huanza kuzeeka na kulegea kadri umri unayoongezeka. Vilevile wanaume wanakoroma zaidi kuliko wanawake hii ni kutokana na wanaume kuwa na njia nyembamba zaidi ya hewa kuliko wanawake.

Kukoroma pia kunaweza kuwa ni tatizo la kurithi. Pombe, kuvuta sigara na matumizi ya baadhi ya dawa pia husababisha misuli ya koo ilegee na hivyo hupelekea mtu akorome. Kulala vibaya pia husababisha kukoroka kama vile kulala kichalichali, kwani hufanya nyama za koo zilegee na kuziba hewa.

 Je, Dawa ya kukoroma ni nini?
Swali hilo limeuliwa sana na mimi katika kulijibu ningependa kusema kuwa, kujua sababu inayosababisha mtu akorome na kuitatua au kuiondoa sababu hiyo ndiko kunakotibu kukoroma. Sote tunajua adha inayotokana na kukoroma, na sauti hiyo inavyosumbua hasa iwapo anayekoroma ni mtu wako wa karibu kama vile mumeo, mwenzi wako au yoyote yule inayekubidi ulale naye karibu au katika kitanda kimojana hata chumba kimoja.

Kukoroma pia huathiri usingizi wa mkoromaji kwani anayekoroka humbidi aamke mara kadhaa usingizini akijua au bila kujua kutokana njia zake za hewa kufunga kwa sekunde kadhaa ambapo usingizi pia hukatika. Wanaokoroma pia hushindwa kulala vizuri suala linalopelekea asubuhi wawe wamechoka na kutofanya majukumu yao vyema, na pia wale wanaolala nao karibu hupatwa na matatizo kama hayo. Vilevile tunapaswa kujua kuwa kukoroma kuna athari za kiafya za muda mrefu kwa mtu anayekoroma hivyo si jambo la kufanyia mzaha na ni tatizo ambalo linapaswa kushughulikiwa na kutatuliwa.

Wataalamu wanatuambia kuwa ili kujua kukoroma kwako kunasababishwa na nini ni bora ushirikiane na mwenzi wako au yoyote unayelala naye ili akuchunguze pale unapolala na kujua jinsi mwili wako unavyokuwa pale unapokoroma. Ni bora aandae orodha na kuchunguza yafuatayo:

1. Kufunga mdomo na kukoroma kunaonyesha kuwa kuna matatizo ya ulimi.

2. Kufungua mdomo na kukoroma kunaonyesha unaweza kuwa na tatizo katika misuli au nyama za koo.

3. Kukoroma unapolala kichalichali kunaonyesha kuwa pengine kwa kubadilisha namna unavyolala kukoroma nako kunaweza kwisha.

4. Kukoroma wakati unapolala kwa kila mlalo kunaonyesha kwamba tatizo lako ni kubwa na pengine kunahitajia tiba kubwa zaidi.

Iwapo umebadilisha namna unavyolala na haikusaidia, unashauriwa ujaribu yafuatayo:

 Punguza uzito
 Safisha njia yako ya hewa. Kuwa na pua iliyoziba hufanya kupumua kuwe kugumu na kusababisha kukoroma. Unaweza kufanya hivyo kwa kutumia dawa za kusaidia kupumua kwa urahisi (nasal decongestants) zinazopatikana kwa urahisi katika maduka ya dawa.
 Wacha kuvuta sigara.

 Lala mapema na pata usingizi wa kutosha kila mara huku ukijiepusha na kuchoka sana. Kunyanyua kichwa kwa nchi 4 huweza kupunguza kasi ya kupumua na kusaidia ulimi na taya kwenda mbele hali ambayo hupunguza kukoroma. Fanya hilo kwa tumia mito maalum ya kupunguza kukoroma au lala bila mto.

Wataalamu pia wanasema kwamba unaweza kupunguza kukoroma kwa kutokula baadhi ya vyakula au dawa kabla ya kulala ambavyo huongeza kukoroma. Vitu hivyo ni kama vile
o Kutokula mlo mkubwa kabla ya kulala.
o Kutokula vyakula vinavyotokana na maziwa au maziwa ya soya.
o Kutokunywa pombe kabla ya kulala.
o Kutotumia dawa aina ya antihistamines.
o Kutotumia vyakula au vinjwaji venye kafeini.

Vilevile wanaokoroma wanashauriwa kufanya mazoezi ya koo ambayo ni pamoja na kuimba, kusoma kwa kurudia rudia voweli (a,e,i,o,u) kwa nguvu kwa dakika tatu mara kadhaa kwa siku, kuweka ncha ya ulimi chini ya meno ya mbele na kurudisha ulimi nyuma kwa dakika 3 kila siku au huku mdomo ukiwa wazi pelekea taya yako upande wa kulia na wacha ibakie katika hali hiyo kwa sekunde 30.

Huku mdomo ukiwa wazi, kaza misuli ya nyuma ya koo na rudia kitendo hicho kwa sekunde thelathini. Unaweza kutizama kwenye kioo na kuona jinsi kilimi kinavyokwenda juu na chini.

Iwapo kukoroma hakutoisha kwa kutumia njia hizo tofauti zilizoelezwa, usife moyo jaribu kumuona daktari na akupe ushauri wa kitiba kuhusiana na tatizo hilo. Madakatari wataalamu wa magonjwa ya pua, masikio na koo au ENT wanaweza kukusaidia zaidi kutatua tatizo hilo.

Siku hizi kuna vifaa mbalimbali vinavyotumiwa mahospitalini ili kuondoa kukoroma kama vile kifaa kinachowekwa kwenye meno, CPAP, kidude kinachowekwa mdomoni au hata kufanyiwa operesheni ili kuondoa tatizo hilo.

Friday, 9 September 2016

Utaratibu wa uhamisho kwa mtumishi wa umma!

UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA

Imetolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

1. Mamlaka za Uhamisho

Kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na 8. ya mwaka 2002 ikisomwa na Kanuni zake pamoja na Taratibu za Uendeshaji za mwaka 2003 Mamlaka ya Uhamisho kwa watumishi wote wa Umma ni Katibu Mkuu Ofisi Ya Rais-Menejimenti ya Utumishi Wa Umma na

Kwa maelekezo ya Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi Wa Umma kwa barua Kumb Na. C/CB.271/431/01/62 ya tarehe 8/06/2006 na Kumb Na. C/CB.271/431/01/J/144 ya tarehe 27/08/2007 Mamlaka ya Uhamisho katika Uhamisho wa watumishi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa yamekasimiwa kwa;

Katibu Mkuu Ofisi Ya Waziri Mkuu TAMISEMI kwa watumishi wanaohama kutoka Halmashauri moja kwenda nyingine nje ya Mkoa;Katibu Tawala Mkoa kwa uhamisho wa watumshi wanaotoka Halmashauri moja kwenda nyingine ndani ya Mkoa na;Mkurugenzi wa Halmashauri kwa watumishi wanatoka kituo kimoja kwenda kingine ndani ya Halmashauri.

2. Aina za Uhamisho

Kuna aina mbili za Uhamisho, nazo ni;

Uhamisho wa Kuomba

Taratibu za Kuomba Nafasi:-

Mtumishi atapaswa kuomba nafasi ya uhamisho kwa kuwasilisha maombi yake ya uhamisho kwa Mkurugenzi wa Halmashauri au Mamlaka anayotaka kuhamia kupitia kwa Wasimamizi wake wa kazi katika kituo chake cha kazi alichopo na Mkurugenzi wake.

Wasimamizi wa mtumishi anayeomba uhamisho watapaswa kuhakikisha maombi ya mtumishi yanafika katika mamlaka husika yakiwa na maoni yao kuhusu maombi hayo na sio kuzuia maombi. Iwapo kutakuwa na sababu ya msingi ya kuzuia maombi mwajiri amjulishe mtumishi kwa kumrejesha katika miongozo iliyopoIwapo Mwombaji hataridhika na maoni /sababu za mwajiri /Msimamizi wa kazi kukataa maombi yake mwombaji atawasilisha maombi yake kwa Katibu Tawala wa Mkoa kwa ushauri na kama hataridhia maombi yatawasilishwa kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI yakiwa na vielelezo muhimu kuthibitisha maombi hayo kukataliwa na Mkurugenzi na kueleza sababu za yeye kuomba uhamisho huo.

Mkurugenzi/Msimamizi wa kazi atayeombwa nafasi ya kuhamia atapaswa kumjibu mtumishi kupitia kwa Mkurugenzi wake kwa barua akimweleza kupatikana kwa nafasi hiyo kumetokana na nini ikiwa ni pamoja na kutaja Check Namba za watumshi waliofariki au kuacha kazi.Iwapo mtumishi wa umma ataomba uhamisho kwa sababu za kumfuata mume au mke, kujiandaa kustaafu baada ya kukaa miaka kumi nje ya mkoa anaotarajia kustaafia na kukaa katika kituo kimoja kwa zaidi ya miaka mitano anaweza kufikiriwa kugharamiwa gharama za uhamisho hata kama ataomba uhamisho mwenyewe.

Mtumishi anayeomba uhamisho atapaswa kuwasilisha maombi yake kwa Katibu Mkuu au Katibu Tawala Mkoa au Mkurugenzi akiambatanisha barua iliyomkubalia kuhamia katika kituo anachotaka kuhamia. Aidha ni muhimu amjulishe mwombaji iwapo atagharimiwa uhamisho au la kufuatia kupata nafasi hiyo

Angalizo:

Hairuhusiwi Mtumishi yeyote kutumia mtu mwingine isipokuwa yeye mwenyewe au Mwajiri wake kwa njia ya posta au Mkono kuwasilisha maombi yake ya uhamisho. Inashauriwa kutumia njia ya EMS au regista kwa urahisi wa ufuatiliaji.

Upatikanaji wa Majibu:-

Watumshi wote walioomba uhamisho watapata majibu yao kwa barua kupitia kwa waajiri wao na sio vinginevyo.Aidha kwakuwa uhamisho huu ni wa wazi watumishi waliokubaliwa au kaukataliwa uhamisho watapata taarifa za awali kupitia Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI yaani www.pmoral.go.tz mapema mwezi Julai kwa maombi yatakayopokelewa kuanzia Januari hadi Juni na mapema mwezi Januari kwa maombi yatayopokelewa kuanzia mwezi Julai hadi Desemba kwa kuwa Ofisi yetu imejipanga kushughulikia masuala ya uhamisho mara mbili kwa mwaka ili kuepusha mwingiliano wa majukumu katika vituo vya kazi kwa mwaka.

Mtumishi atakayekuwa na malalamiko kuhusu maombi yake ya uhamisho anashauriwa kuelekeza maombi yake kwa Mamlaka iliyomwamisha kupitia kwa mwajiri wake na msimamizi wa kazi akiambatisha maombi yake ya awali na vilelezo vingine muhimu kama sababu za kuomba uhamisho na ushahidi wa kufikisha barua yake kwa Mamlaka ya uhamisho.Malalamiko ya mtumishi aliyeomba uhamisho na hakupata majibu au hakuridhika na majibu aliyopatiwa malalamiko yake yatashughulikiwa ndani ya siku saba bila kujali muda wa uhamisho yaani June au Desemba.

Baada ya mtumshi kupata majibu /barua ya uhamisho atapaswa kuripoti ndani ya siku kumi na nne tangu amekabidhiwa barua yake ya uhamisho vinginevyo atachulikuliwa ni mtoro kazini.Uhamisho wa Kawaida

Uhamisho huu ni wa kawaida ambapo Mwajiri au Msimaimizi wa kazi anafanya uhamisho kwa sababu za kuboresha utendaji.

Hata hivyo ili uhamisho huo ufanyike pia Mamlaka za uhamisho zinatakiwa kujiridhisha uwepo wa nafasi wazi katika Halmashauri anayohamishiwa mtumishi wa hakusababishi upungufu katika Sehemu mtumishi anakotoka au anakohamia.

Uhamisho huu kwa kawaida unagharamiwa na Halmashauri inayompokea mtumishi na ile inayomruhusu kwa kumlipa gharama za kufunga mizigo kama ilivyoelezwa kwenye Kanuni L (8 na 13) ya Utumishi wa Umma ya Kudumu toleo la 2009 na marekebisho yake ya mwaka 2010 kwa wakati. hivyo ni muhimu Mamlaka za Uhamisho kijiridhisha na uwezo wa Halmashauri kugharamia uhamisho huo ili kuepuka kuzalisha madeni kwa Serikali

Pamoja na utaratibu wa uhamisho kuwa ni uhamisho kufanyika mara mbili kwa mwaka, uhamisho huu wa kawaida unaweza kufanyika wakati wowote katika jitihada za kunusuru utendaji katika kituo alichopo mtumishi au anachohamishiwa mtumishi kwa manufaa ya umma.

Angalizo:

Mtumishi atakayebainika kughushi saini za viongozi, kuomba au kupokea rushwa katika ngazi yoyote atachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kumfikishwa mbele ya vyombo vya dola kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria.

Ni muhimu kwa Waajiri kujiridhisha na majibu ya barua za uhamisho kutoka katika Mamlaka za uhamisho ili kuona kama maombi yake yalifuata taratibu sahihi na watumishi waliopata majibu wanatayarishiwa mapema data sheet na kumbukumbu za utumishi na mshahara ili kuepusha usumbufu kwa watumishi na waajiri wanaowapokea watumishi

Mambo 10 ambayo mwanaume hupenda kusikia toka kwa wenzi wao!

Fahamu Mambo 10 Ambayo Mwanaume Hupenda Kusikia Toka Kwa Mpenzi Wake!

10. Kukosolewa – “I think you are wrong”

Wanaume wanaweza kujikweza sana lakini daima hawachukii kurekebishwa. Wanachojali zaidi ni jinsi gani au njia gani imetumika kuwarekebisha. Mwanaume akikosea, anataka mpenzi wake amkosea lakini kwa mapenzi, sio kwa mikwaruzano au dharau au mbele ya kadamnasi. Mrekebishe au mkemee faragha, toa maoni yako na wala usimlazimishe, itamfanya aone unajali na unataka kumjenga.

9. Kujali – “How was your day?”

Wanawake wengi hutaka wao tu ndio waulizwe kuhusu jinsi siku zao zilivyoenda kila siku, wanasahau kabisa hata wanaume nao walikua kwenye mihangaiko. Mzoeshe kumuuliza mpenzi wako siku yake ilikuwaje? utaona hata nuru ya mapenzi yenu itang’aa na mtakua marafiki, japo mwanzoni atakua hakuambii kila kitu lakini baada ya muda atazoea. Kila mtu anataka wa kumsikiliza, mtu atakayezungumza nae chochote kilichotokea ndani ya siku yake, na pengine kukuuliza ushauri.

8. Ucha Mungu – “Can we pray?”

Mwanaume, anayesali au kutosali, lazima huwa ana imani kwamba Mungu yupo. Mwanamke mcha Mungu siku zote huwa ni wazo la kila mwanaume endapo ana mpango wa kuoa. Mwanaume huwa na amani kwa kiasi fulani akiongozwa na mwanamke wake kwa upande huo wa sala.

7.  Msamaha – “I forgive you”

Vikombe kwenye sahani havikosi kugongana, vivyo hivyo na kwa wapenzi, kuumizana hisia hakuepukiki, iwe kwa makusudi au bahati mbaya, mwenzio akikosea sasa isiwe ndo adhabu, akiomba msamaha ukamwambia nimekusamehe na kweli umemsamehe, funika kurasa endeleeni na maisha. Usililete tena mezani jambo ulilosema umesamehe.

6. Sifa – “That was great sex”

Kama amefanya kazi nzuri, mwambie. Wote tunajua sio kila siku watu hufanya kiwango che Maradona au Pele, siku akiwa kwenye kiwango hicho hata yeye anajua, usisite kumpa sifa zake. Wazungu wanasema, ‘Yes, you can kiss and tell some of the times’. Na kama unaona kuna sehemu anahitaji kujisogeza, mwambie pia, tena kimahaba. Hii itawasaida nyote.

5. Upekee  – “I admire you. No other man is like you”

Ni kweli kwamba kuna wanaume ambao ni wazuri na wenye uwezo mkubwa zaidi ya huyo ulienaye, lakini kwake hujisikia vyema zaidi ukimwona yeye ni zaidi ya wote hao. Sio mbele ya macho yake tu, matendo yako na hata nyuma yake msifie kwamba yeye ndio mwanaume pekee duniani unayempenda na hakuna mwingine zaidi yake.

4. Uaminifu – “I trust you”

Mwanaume akijua anaaminika sana kwa mwanamke, na yeye hujiachia. Na kwa hili huwa anaweza kugombana na watu kabisa kwa ajili ya mwanamke wake. Japo wengine hulitumia hili kwa uchafu wao lakini wengi wao ni kitu chema kwao.

3. Mapenzi –  “Make love to me”

Ni mtazamo wa wengi kwamba mwanaume ndio siku zote awe mwanzilishi wa tendo. Lakini mwanaume kwa wakati mwingine hupenda mwanamke wake ampe vishawishi na yeye vya kumleta kwenye mood. Sio kila siku aanze yeye tu, wakati tendo ni la kuwafurahisha wote. Hata kama ni ngumu kusema kwa mwanamke, ishara kibao zipo za kumuonyesha mwenzi wako akaona ‘Leo baby anataka na yeye’.

2. Malengo -“What’s your dream?”

Mwanaume anaweza asionyeshe kama anahitaji msaada, lakini kwa kutumia njia za mapenzi, unakuta ni mwanaume tu anayehitaji uwepo  wa mwanamke anayempenda yeye. Mungu alimtengeneza mwanaume na kumpatia msaidizi kwa kumpatia mwanamke. Kuwa mwanamke mwenye msimamo na mpangilio mahiri usiotikisika, ambaye unauwezo wa kumuuliza anaenda wapi katika maisha yake, na akakukumbusha huko siko ni huku. Ndoto za mwanaume mara nyingi huendana na zile na mwenzi wake, na mwanamke huwa pale kuhakikisha ndoto za pamoja zinatimia.

1. Upendo wa dhati – “I love you”

Wanaume wengi hujiona wagumu kwenye kutamka neno ‘I love you’ kwa wanawake zao na hata akisema itakua ni mara chache chache hata kama kweli kutoka moyoni wanapenda, lakini haina maana hawataki kuambiwa na watu wanaowapenda, hii huwaaminishia nafasi yao kwenye moyo wa mwanamke.

Monday, 5 September 2016

Mambo 10 muhimu maishani

Katika dunia ya leo, ambayo ipo kwenye ushindani mkubwa ili uweze kufanikiwa unalazimika kujifunza mambo mengi ya kukusaidia kufanikiwa huko. Bila kufanya hivyo hautaweza kufanikiwa na kufikia viwango vya juu, zaidi utaishia kuwa na mafanikio ya kawaida kabisa.

Haijalishi uwe umeajiriwa au umejiajiri ni muhimu kujua mambo mengine ya ziada ambayo tena ni ya kawaida lakini, yanaendana na kasi ya ulimwengu wa sasa. Kwa jinsi utakavyojua mambo hayo utazidi kujiongezea thamani kubwa ambayo bila ubishi itazidi kukupa mafanikio.
Yafuatayo Ni Mambo 10 Ambayo Ni Muhimu Kuyafahamu Kwenye Maisha Yako.

1. Kuongeza maarifa.
Kila siku na kila wakati, jenga tabia ya kuongeza maarifa. Jifunze kupitia vitabu au semina mbalimbali. Kuunoa ubongo inatakiwa iwe sehemu ya maisha yako na  ni hatua muhimu sana ya kukusaidia kufikia mafanikio makubwa kuliko unavyoweza kuwaza au kufikiri. Watu wenye mafanikio wanajifunza sana kila siku.

Ongeza maarifa yako kila siku.

2. Kutengeneza bajeti.
Huhitaji kusomea uchumi ndio uweze kupanga bajeti. Katika maisha yako pia unahitaji kujifunza juu ya upangaji wa bajeti zako binafsi. Hiyo itakusidia kutokuwa na matumizi ya hovyo ya pesa zako. Pia bajeti itakusaidia kutunza pesa na kukusaidia kuwekeza kwa siku za baadae.

3. Kuwasikiliza wengine vizuri.
Ni vyema kujua namna ya kuwasikiliza wengine vizuri. Acha kuwa muongeaji tu kila wakati na kusahau kuwasikiliza wengine. Unapowasikiliza wengine inakusaidia kujifunza mambo ya msingi ambayo ingekuwa sio rahisi kwako kujifunza kama ungekuwa unaongea wewe tu.

4. Kongea mbele ya watu wengine.
Jambo lingine ambalo hutakiwi kukwepa kujifunza ni kuongea mbele za watu. Lazima uwe na maarifa ya kukusaidia kuogea mbele za watu. Ikiwa utakuwa unaogopa kuongea mbele za watu jiulize, ni nini kitatokea ikiwa utapewa jukumu hilo? Hivyo unalazimika kujifunza hili pia kwa faida yako.

5. Kujifunza lugha zingine.
Kwa dunia ya sasa jinsi ilivyo, si ya kukaa na kujivunia lugha ya aina moja. Ni vizuri ukawa na tabia ya kujifunza lugha nyingine za kigeni angalau hata moja pole pole. Hiyo itakusaidia hasa pale unapotaka kujifunza kitu kwa mfano kupitia vitabu haitakuwa tabu sana kwako kwa sababu lugha utakuwa unaijua.

6. Kuwa na mwonekano mzuri.
Moja ya kitu kizuri cha kukusaidia kukutambulisha ni mwonekano mzuri ulionao. Unapokuwa na mwonekanao mzuri inakusaidia kukutambulisha wewe ni nani. Pia Mwonekano wako unakuwa unakutangaza kwamba wewe ni mtu wa aina gani katika jamii husika.

7. Kulinda siri za wengine.
Ni vyema katika maisha ukajifunza pia kuwa mtu wa kutambua na kulinda siri za watu wengine. Usiwe mwongeaji sana wa mambo yasiyo kuhusu hasa ya watu wengine. Linapotokea jambo ambalo unaona linaweza likawa siri, ni vyema kukaa kimya kuliko ukawa mvujishaji wa mambo ya watu.

8. Kutumia kompyuta kwa ufasaha.
Haijalishi wewe ni bosi au muajiriwa. Ni muhimu sana kujifunza juu ya matumizi ya kompyuta. Hapa unatakiwa ujue program mbalimbali kama ‘Microsoft office au Excel’ ambazo zinaweza kukusaidaia. Pia kwa kujua kompyuta hata ikitokea umepata kazi sehemu, zipo ofisi ambazo hazihitaji sana secretary maarifa hayo yatakusaidia.

9. Kuendesha gari.
Unaweza ukaona ni kitu cha kawaida lakini lazima ujue kuendesha gari. Hii sio dunia ya kusubiri eti ununue gari ndio ujue kuendesha. Ni muhimu kujifunza kuendesha gari na hiyo itakusaidia kukuongezea wasifu kwenye mambo mengine kama ya kazi au kukupa uzoefu binafsi hata wewe.

10. Kupika.
Si vibaya ukawa na maarifa ya kupika pia. Haijalishi wewe ni mwanume au mwanamke ni muhimu kujua kupika hata kidogo. Jiulize kama hutaki kabisa kupika wale wanaokupikia siku wasipofanya hivyo utafanyaje? Naamini itakusumbua na itakuwa shida kwako. Hivyo ni muhimu kujua kupika na hilo jukumu lisibaki kwa wanawake tu hata kwa wanaume pia.

Hayo ni baadhi tu ya mambo machache ambayo unalazimika kuyafahamu katika maisha na mafanikio yako kwa ujumla. Unaweza ukajifunza mambo mengine zaidi kwa kadri unavyoweza.

Sunday, 4 September 2016

Majambazi yafanya tukio lingine!

Majambazi, hii sasa imezidi! Tunaomba serikali iangalie hili kwa jicho pevu!

Handeni. Siku moja baada ya majambazi kumuua mlinzi katika Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (Sekomu), Tanga, majambazi ambao idadi yao haijafahamika, wamefunga Barabara ya Segera – Chalinze katika Kijiji cha Kwachuma wilayani Handeni kwa zaidi ya saa mbili na kupora fedha na simu za abiria waliokuwa kwenye magari usiku wa kuamkia jana.

Katika tukio hilo, watu watano walijeruhiwa kwa mapanga na kupelekwa Hospitali ya Magunga Korogwe.

Juzi, majambazi yalivamia Sekomu na kulipua moja ya mabweni ya chuo hicho, kisha  kumuua Mlinzi wa Kampuni ya Ulinzi ya Tele Security, Yohana Shemzigwa na kumjeruhi mlinzi mwenzake, Abuu Rajab.

Akizungumzia tukio la usiku wa kuamkia jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba alisema majambazi hao walifunga barabara saa tano usiku kwa kutumia magogo kisha kuanza kuwapora mali watu waliokuwa wakipita kwa magari eneo hilo.

Friday, 2 September 2016

Mawe katika kibofu cha mkojo!

Tatizo la mawe katika kibofu cha mkojo (Gallstones).

Tatizo hili linazidi kushika kasi kwa kuwasumbua watu wengi kuliko ilivyokuwa awali. Vitu kama mitindo ya maisha na vyakula tunavyokula, vinatajwa kuwa chanzo kikuu cha tatizo hili.

Kwa kuzingatia hilo, makala haya yameandaliwa kujaribu kuchambua Gallstones ni nini, husababishwa na nini na matibabua yake.Gallstones ni nini?

Gallstones ni vimawe vidogovidogo vinavyopatikana kwenye kibofu cha mkojo au kwenye nyongo ambavyo humsababishia mgonjwa maumivu makali. Vimawe hivi vinaweza kugawanywa katika makundi makuu matatu.

Cholestrol Gallstones (Mawe ya Lehemu)

Haya husababishwa na ulaji uliokithiri wa vyakula vyenye Cholesrtol ambapo ikiingia kwenye mzunguko wa damu, hujikusanya na kisha kuganda kwenye kibofu ambapo baada ya muda hubadilika na kuwa vimawe vigumu.

Black Pigment ( Pigmenti nyeusi)

Haya husababishwa na kuharibiwa kwa kiwango kikubwa cha chembe nyekundu za damu (red blood cell) ambapo mabaki ya seli hizo hujikusanya kwenye kibofu na kuganda, kisha kutengeneza vimawe vigumu vyenye rangi nyeusi.

Brown Pigment (Pigmenti za Kahawia)

Haya husababishwa na kurundikana kwa uchafu katika kibofu cha mkojo. Wanywaji wa pombe na wavutaji wa sigara wapo katika hatari kubwa ya kupata aina hii ya mawe kwenye kibofu.Uwepo wa mawe haya kwenye kibofu husababisha maumivu kama ya moto kuwaka tumboni, tumbo kujaa gesi na kunguruma, mwili kukosa nguvu, homa kali na kama mgonjwa asipotibiwa, husababisha kifo.

DALILI ZA TATIZO!

Tatizo hili linapoanza, huwa hakuna dalili za moja kwa moja, na mtu anaweza kukaa na mawe hayo kwa miaka kadhaa bila kuhisi chochote. Dalili huanza kuonekana yanapoongezeka ukubwa na kufikia kiwango cha milimita 8. Dalili za awali huwa ni kuhisi maumivu makali upande wa kulia, juu ya tumbo.

Maumivu haya huambatana na
kichefuchefu cha mara kwa mara na kutapika mfululizo. Dalili nyingine ni maumivu makali katikati ya mabega, upande wa mgongoni hasa nyakati za usiku.Pia kushindwa kula vyakula vyenye mafuta ni dalili nyingine ya tatizo hili.

Mtu mwenye mawe kwenye kibofu, anapokula chakula chenye mafuta, hata kwa kiwango kidogo, hupatwa na kichefuchefu, tumbo hujaa gesi na wakati mwingine hutapika nyongo.

MADHARA.

Uwepo wa mawe katika kibofu, husababisha ugonjwa uitwao Cholecystitis ambao huendana na kurundikana kwa nyongo katika kongosho, hali ambayo husababisha tatizo lingine la utumbo kushambuliwa na bakteria hususan Escherichia coli au Bacteroides.

Mawe haya husababisha madhara zaidi kwa kuziba mirija mbalimbali ndani ya mwili, ikiwemo mirija ya mkojo, hali ambayo kitaalam huitwa Cholangitis au Pancreatitis.

Hali hizi huwa hatari sana kwa uahi na husababisha kifo kwa mgonjwa endapo atachelewa kupatiwa matibabu

UCHUNGUZI WA TATIZO

Ugonjwa wa mawe katika kibofu au nyongo, hupimwa kwa kutumia mbinu za kitaalam ambazo ni:
Ultrasound: Mionzi maalum hutumika kuangalia viungo vya ndani ya tumbo, hasa kibofu na nyongo kuangalia kama kuna vitu visivyo vya kawaida. Majibu ya Ultrasound pekee hayatoshi kutoa majibu ya mwisho, bali daktari atayaunganisha na majibu ya vipimo vingine.

Oral Cholecystogram (OCG): 
Hii ni mbinu ambayo mgonjwa anapewa vidonge maalum ambavyo vikigusana na mawe ndani ya tumbo, hubadilika rangi na kufanya iwe rahisi kwa mawe hayo kuonekana kwenye kipimo cha tatu,

X- Ray.
X Ray: Baada ya mgonjwa kumeza vidonge, picha za X Ray zikipigwa huonesha mahali mawe yalipo, ukubwa na jinsi yalivyokaa.
Baada ya vipimo hivi, daktari anaweza pia kushauri mgonjwa apimwe damu ili kupata taarifa kamili juu ya afya yake.

MATIBABU!
Hakuna matibabu ya moja kwa moja ya tatizo hili. Baada ya uchunguzi wa tatizo, daktari na mgonjwa wataamua mbinu ya matibabu inayofaa lakini kama hali ya mgonjwa ni mbaya, hakuna mbinu nyingine inayoweza kufaa zaidi ya upasuaji ambapo kifuko cha nyongo hukatwa na kutolewa kabisa!

Kama mgonjwa ana hali ya kawaida, tiba mbadala kama kufunga (fasting), kunywa maji na juisi kwa wingi, kuepuka vyakula vyenye mafuta na sukari kwa wingi, husaidia sana kupunguza athari za ugonjwa huo.

Dawa za Acetaminophen pia hupunguza maumivu ingawa ni kwa muda.