Wednesday, 31 August 2016

Kupatwa kwa jua, chukua tahadhari!

Tukio la kupatwa kwa jua nchini Tanzania kushudiwa!

Tahadhari imetolewa kwa wakazi wa mikoa ambayo itashuhudia kupatwa kwa jua kuwa kutazama jua moja kwa moja bila kutumia kifaa chochote kunadaiwa kuwa na madhara kwa mtazamaji kutokana na mionzi ya jua hilo.

Kupatwa kwa jua kunatarajiwa kutokea katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ya Njombe wilaya ya Wang'ing’ombe katika kijiji cha Litundu, Mbeya wilayani Mbarali katika kijiji cha Mpungarelini na mkoani Katavi ambako kupatwa kwa jua kutaonekana vizuri kwa zaidi ya asilimia 97.

Tahadhari hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Njombe Dkt. Rehema Nchimbi wakati akiongea na waandishi wa habari mkoani humo ikiwa zimebaki siku chache kutokea kwa tukio hilo la kihistoria.

Mkuu wa Mkoa huyo amesema kuwa kuna jitihada mbalimbali zinazofanywa na halmashauri ya Waning'ombe kwa ajili ya kuweza kupata vifaa mahususi kwa ajili ya kushuhudia tukio hilo bila kuacha madhara yoyote.

Tukio hilo la kupatwa kwa jua lilizinduliwa Julai 10 mwaka huu katika kijiji cha Litundu kwa mkoa wa Njombe ambapo macho ya dunia nzima kitalii yatatazama katika eneo hilo.

Polisi wapiga kambi Ofisi ya Chadema!

Polisi wapiga kambi Chadema

NI mwendo wa doria. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya askari polisi kulazimika kupiga kambi katika Ofisi za Makao Makuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), zilizopo Mtaa wa Ufipa, Dar es Salaam.

Polisi hao tangu jana asubuhi walikuwa wakifanya doria katika eneo hilo huku wengine wakizingira ofisi za chama hicho wakiwa wamevaa kiraia.

Kutokana na hali hiyo, MTANZANIA ilituma timu ya waandishi ambao kutwa nzima ya jana waliwashuhudia askari polisi wakiwa nje ya ofisi za chama hicho na wengine wakiwa ndani ya magari ya doria.

Hatua hiyo ilionekana kuzua taharuki kwa baadhi ya wanachama na viongozi wa juu wa chama hicho ambao walijikuta wakishindwa kufanya kikao cha dharura cha Kamati Kuu kwa hofu ya kuzuka vurugu.

Ilipotimu saa tano asubuhi, timu ya walinzi wa Chadema ‘Red Brigade’ waliongezeka na kusimama nje ya ofisi za makao makuu huku wakionekana kuwa tayari kwa lolote, ikiwamo kujihami kwa kuwalinda viongozi wao; mawaziri wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye ambao waliwasili katika ofisi hizo kwa ajili ya kikao.

Kikao hicho kilikuwa ni cha mwandelezo baada ya kile cha juzi kushindwa kumalizika na baadhi ya viongozi wa chama hicho kukamatwa na polisi.

Pamoja na hali hiyo, ilipotimu saa 9 alasiri, viongozi hao wakiongozwa na Lowassa walitoka nje na kuelezwa kuwa kikao kimeshindwa kufanyika kwa kuwa hali ya usalama si nzuri, hasa baada ya kuonekana askari kanzu wakiingia ndani ya ofisi hiyo na wengine kujifanya ni wanachama wa chama hicho.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe pamoja na Katibu Mkuu, Dk. Vicent Mashinji, walilazimika kuondoka mapema na kwenda katika kikao cha pamoja kati yao na viongozi wa dini ili kutafuta mwafaka, kuhusu Operesheni Ukuta inayotarajiwa kufanyika kesho licha ya kuzuiwa na Jeshi la Polisi.

Kikao hicho cha viongozi wa dini kilichofanyika katika Hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam, pamoja na mambo mengine kilijadili kwa kina mkwamo wa kutafuta suluhu kati ya viongozi wa Chadema na Serikali kuhusu kuzuiwa maandamano ya kesho.

MTANZANIA ilipomtafuta Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Mashinji ili kupata ufafanuzi kuhusu kuzingirwa kwa ofisi zao na maofisa wa polisi, alikiri kutokea kwa hali hiyo.

“Ni kweli tumeahirisha mkutano wetu wa Kamati Kuu mpaka hapo baadaye, Ofisi zetu za Makao makuu zilizingirwa na askari wa kila aina, wengine walivaa baraghashia, kanzu na kila aina ya nguo kwa lengo la kuvunja na kutawanya mkutano wetu wa ndani, tumeuahirisha mpaka wakati mwingine, tutawajulisha.

“Askari hao wamekuwa wakipiga kambi katika ofisi zetu kwa muda wa wiki sasa, lakini kadiri siku zinavyokwenda idadi yao inazidi kuongezeka kama ilivyokuwa leo (jana),” alisema Dk. Mashinji.

Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho zilieleza kuwa wajumbe wa Kamati Kuu walikutana ili kujadili mambo mbalimbali ikiwamo suala la maandamano yanayotarajiwa kufanyika nchi nzima kuanzia kesho.

VIONGOZI WA DINI

Viongozi wa dini nchini wameendelea kukuna vichwa kutafuta suluhu kati ya Serikali na vyama vya siasa vinavyojiandaa na Operesheni Ukuta iliyopangwa kufanyika kote nchini kesho.

Viongozi hao walijichimbia jana Hoteli ya Courtyard katika kikao cha siri ambacho kilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Chadema, Mbowe, Katibu Mkuu wake, Mashinji na mawaziri wakuu wa zamani; Sumaye na Lowassa.

Taarifa za ndani zinasema kuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana aliwasili hotelini hapo saa nne asubuhi, lakini aliondoka punde baada ya kupokea simu ambayo inadaiwa alipigiwa na Rais Dk. John Magufuli.

Kikao hicho kilichoanza saa mbili asubuhi hadi saa tisa alasiri ni cha tatu kufanyika, ambacho mbali kuhudhuriwa na viongozi dini, pia kilihudhuriwa na vyama vitano vyenye uwakilishi bungeni huku agenda kuu ikiwa ni hali ya kisiasa nchini.

Akizungumza na MTANZANIA, Mwenyekiti Mwenza wa mkutano huo, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, alisema kuwa ulimalizika salama na kukubaliana na kwamba watatoa taarifa rasmi ya kikao hicho leo kwa umma.

“Kikao chetu tunamshukuru Mungu tumemaliza salama na kwa pamoja tumeweza kukubaliana mambo mbalimbali, ikiwamo ya hali ya kisiasa nchini, wabunge wa upinzani kususia vikao vya Bunge pamoja na Operesheni Ukuta, ambayo tutayazungumza kwa waandishi wa habari kesho (leo) ili Watanzania waweze kuyajua,” alisema Sheikh Alhad.

Pamoja na mambo mengine, alisema kwa sasa hali ni nzuri na wanaamini mkutano huo utaweza kurudisha hali ya utulivu, umoja na mshikamano kwa wananchi wote bila ya kujali tofauti zao za kisiasa, dini au kabila.

KAULI YA MASAJU

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa mkutano huo, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Fredrick Shoo, aliliambia MTANZANIA kuwa Serikali iwaache wafanye mambo kwa wakati wanaoona unafaa.

Dk. Shoo alikuwa akizungumzia kauli iliyotolewa juzi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, akiwataka viongozi wa dini kuliombea taifa lisiingie kwenye uvunjifu wa amani kutokana na Operesheni Ukuta na kwamba huu si wakati mwafaka wa kukaa meza ya majadiliano.

“Sisi tunafanya vitu kwa wakati tunaoona unafaa, siyo yeye atuamuru cha kufanya, namuomba ayaache haya mambo hivi hivi kwani tunaujua wajibu wetu kwa Serikali na wananchi ambao ni waumini wetu.

“Kwa sasa haya mambo tuyaache yabaki kama yalivyo, sisi tunazungumza kuhusu masuala hayo hayo na tumefikia mahali pazuri, mtayasikia kesho (leo), bado kikao hakijaisha,” alisema Dk. Shoo.

Monday, 29 August 2016

Lema agoma kula!

Lema Aendelea Kugoma kula akiwa mahabusu.

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), ameendelea kugoma kula kwa siku ya tatu mfululizo tangu alipokamatwa Oktoba 26 mwaka huu, nyumbani kwake mjini hapa, akidaiwa kutoa maneno ya uchochezi.

Lema alikamatwa siku hiyo saa 12 alfajiri akiwa nyumbani kwake, Njiro,  na hadi sasa anashikiliwa katika mahabusu ya kituo kikuu cha polisi mjini Arusha.

Kutokana na kuendelea kugoma kula, Wakili wake, John Mallya amesema leo saa sita mchana atakwenda Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha kufungua kesi ya kutaka mteja wake afikishwe mahakamani.

Malya jana alisema katika kesi hiyo atashirikiana na Chadema kuwashtaki mwendesha mashitaka mkuu wa Serikali na mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai, Mkoa wa Arusha.

Tangu mbunge huyo akamatwe amegoma kula kwa  kile anachodai kupinga udhalilishwaji aliofanyiwa na polisi wakati wa kukamatwa.

Pia, Lema anasema alinyanyaswa mbele ya watoto wake nyumbani kwake huku wakijua yeye ni kiongozi na amechaguliwa na wananchi.

Neema, mkewe Lema,jana alithibitisha kwamba  mumewe amegoma kula.

“Anaendelea kugoma kula mpaka sasa kwa sababu  hata sasa nimetoka polisi asubuhi kumpelekea chakula, lakini amekataa kula.

“Lakini nilipouliza pale polisi kuwa wanampeleka lini mahakamani, nilijibiwa wanaendelea kumhoji,”alisema Neema.

Juzi, Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, alithibitisha kukamatwa kwa Lema na kueleza kuwa alihojiwa dhidi ya matamshi ya uchochezi na kuwa atafikishwa mahakamani baada ya kukamilika   uchunguzi.

Kwa mujibu wa Kamanda Mkumbo, Lema anatuhumiwa kuwachochea wakazi wa Arusha kuandamana Septemba mosi, mwaka huu kuhamasisha kile kinachoitwa Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta).

Thursday, 25 August 2016

Mwanafunzi ampa mimba mwalimu wake, atuzwa milioni 600.

Mwanafunzi atunzwa M600 kwa kumpachika mimba mwalimu.

Mahakama moja ilimtunuku mwanafunzi Sh600 milioni kwa kumtia mimba mwalimu wake akiwa na miaka 16

–Mwalimu huyo alifungwa kwa mwaka mmoja lakini alikaa jela kwa miezi sita pekee. Binti wao ana miaka mitatu

Mwanafunzi mmoja California, Marekani, atatunzwa Sh600 milioni kwa kuhusika kimapenzi na mwalimu wake na kumtia mimba.

Mwalimu huyo Laura Whitehurst, 31, alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na kijana huyo akiwa na miaka 16 ambapo alipata mimba na kumzalia binti miezi tisa baadaye.

Hukumu hiyo ilitolewa miaka mitatu baada ya Whitehurst kutambulika kuwa alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanafunzi wake.

Mahakama iliambiwa kuwa mwalimu huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi wengine wawili ambao hawakutambulishwa.

Ilisemekana mwalimu huyo alikuwa akishiriki ngono darasani akiwa na mvulana huyo, na nyumbani kwake kwa mwaka mmoja kabla ya tukio hilo kujulikana.

Mwanafunzi huyo alidai kuwa usimamizi wa shule yake, Redlands Unified School District, ulikuwa ukijua kuhusu uhusiano huo lakini ukakataa kuchukua hatua yoyote.

“Ushahidi unaonyesha kuwa usimamizi ulijua vyema kuhusiana na suala hilo lakini ukakataa kuchukua hatua yoyote,” alisema wakili wa mwanafunzi huyo Vince Finaldi.

Whitehurst alifungwa mwaka mmoja 2013 kuhusiana na kisa hicho lakini alikaa jela kwa miezi sita pekee kwa kuonekana kuwa na tabia njema.

Have a nice day all my viewers!!

Wednesday, 24 August 2016

UDOM na wataalamu wa mafuta na gesi.

UDOM kuongeza wataalam wa mafuta na gesi.

Chuo Kikuu cha UDOM kimeandaa mtaala wa elimu kwa ajili ya shahada ya uzalimili katika sekta ya mafuta na gesi ili kutoa watalaam wengi zaidi wa masuala ya athari za kimazingira zinazoweza kusababishwa na uchimbaji wa rasimali hiyo.

Kaimu Makamu mkuu wa chuo hicho Dkt. Peter Msofe amesema hayo mjini Dodoma katika uifunguzi wa mkutano wa wadau wa elimu kutoka nchi za Uganda na Tanzania wanaoandaa mtaala wa unaolenga kuzinufaisha nchi mbalimbali za Afrika.

Dkt. Msofe amesema kuwa mtaala huo umekuja wakati muafaka wakati Tanzania imegundua gesi nyingi hivyo kuna uhitaji wa watalaam ambao wataweza kujua faida na athari za rasimali hiyo kimazingira na kiafya nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitivo cha Sayansi Asilia na Hisabati Said Ali Vuai, amesema kuwa mtaala huo unatarajiwa kuanza katika mwaka wa masomo 2017/2018.

Together we can, yes we can!

Saturday, 20 August 2016

Fanya haya ufikie malengo yako!

Mambo 8 Yatakayosaidia Kufikia Malengo Yako.

Kila wakati wengi wetu katika maisha, ni watu wa kujiwekea malengo. Mara nyingi huwa tunaweka malengo haya,  kwani kwa kujiwekea  malengo hayo ndiyo hutuongeza na kutuhakikishia  kule tunakotaka kufika kimafanikio. Kwa kujua hili, karibu kila mtu msaka maendeleo, kwake malengo huwa ni kitu cha lazima sio cha kuuliza tena.

Lakini hata hivyo, pamoja na kujiwekea malengo mazuri,  kwa bahati mbaya sana tena wengi wetu huwa bado hatuyafikii malengo hayo. Hapo ndipo maswali mengi sana ya kwanini huanza kuibuka vichwani kwetu? Kama mambo ni hivyo usikate tamaa, Kwa kufatilia makala haya utajifunza juu ya mambo muhimu yatakayokusaidia kufikia malengo yako.

1. Yajue malengo yako vizuri.                                                                      
Huwezi kufanikiwa kama huyajui malengo yako vizuri. Ni lazima malengo yako yawe ya wazi kwako. Ikiwezekana yaandike vizuri kwenye karatasi nayaweke sehemu inayoonekana. Kwa mafano kama lengo lako ni kufanya biashara ya ‘stationary’ liandike lengo hilo mahali na lionekane.  Kama pia lengo lako ni kufungua duka weka wazi lengo lako kwa kuliandika.

Watu wengi mara nyingi wanashindwa kufikia malengo yao kwa sababu malengo yao yanakuwa sio wazi sana. Siku zote mawazo yetu ya ndani hutusaidia kufikia malengo yetu, kama malengo hayo yana eleweka. Kinyume cha hapo, utakaa sana kusubiri malengo yatimie lakini wapi. Hivyo siri ya kufikia mafanikio jitahidi kuweka malengo yako wazi.

2. Jitoe kikamilifu.
Siri ya mafanikio ni kujitoa kikimalifu kwa kile unachokifanya. Hata malengo yako ambayo umeshajiwekea na yako wazi ili kuweza kuyafikia ni lazima ufanye juu chini kujitoa kikamilifu na wala sio nusunusu. Ikiwa utakuwa unayaendea malengo yako, huku ukiwa hujaamua kujitoa kikamilifu tambua ikatokea umeshindwa usishangae hapo kwa hilo.

Kwa kuwa unanajua malengo yako nini, kama kuna kazi unatakiwa kuifanya ifanye kweli kwa nguvu zako zote bila kuchoka. Weka juhudi na maarifa yako yote na kuhakikisha unajitoa kweli. mafanikio yako hayatakuja kirahisi eti kwa kufanya kazi kilegevu. Jitoe kwa kupiga kazi kwelikweli mpaka kieleweke.

3. Kamilisha majukumu yako kila siku.
Unaweza ukawa unayajua malengo yako na umejitoa kikamilifu, lakini huwezi kuyafikia malengo yako kama kila wakti unakuwa hukamilishi zile kazi zinazotakiwa  kukusaidi kuyafikia malengo yako. Hapa sasa ndipo unapotakiwa kujilazimisha na kuhakikisha kila jukumu ulilonalo  unalikamilisha  kwa siku husika.

Kwa mfano kama wewe ni mfnyabiashra ulitakiwa kupga mahesabu Fulani ya kukusidia, fanya hivyo bila kuacha. Halikadhalika akama wewe ni mwandishi na umejipangia kuandika kurasa mbili kwa siku, pia fanya hivyo bila kuacha wala kuahirisha. Kwa kukamilisha majukumu yako kila siku itakusaidia kufikia malengo yako kuliko ambavyo ungefanya mambo nusunusu.

4. Yagawanye malengo yako.
Malengo yoyote ulinayo yanaweza kufikika. Haijalishi malengo hayo ni makubwa kivipi lakini uwezo wa kuyafanikisha upo, ikiwa tu lakini utafuata hatua za kuyakamilisha malengo hayo. Pengine unajiuliza kivipi au nitawezaje kuyakamilisha malengo yangu makubwa? Ni rahisi tu na hata wewe unaweza.

Kulielewa hilo vizuri ngoja nikupe kisa kimoja moja ambacho kinaelezea siku moja fisi mkubwa alimkuta fisi mdogo akimla tembo. Fisi Yule alivyoona vile alicheka sana na kumuuliza utamaliza lini? Fisi Yule mdogo alimwambia nitamla kidogo kidogo mpaka ataisha. Kwa kutumia mfano huo hivyo, ndivyo unavyotakiwa na wewe kufanya kwa malengo yako makubwa. Unajiona una malengo mkubwa yagawe vipande vipande mpaka uyafikie..

5. Tafuta msaada.
Ni rahisi kuyafikia malengo yako, kama utatafuta msaada wa kukusaidia kuyafikia malengo hayo. Acha kung’ang’ania kukamilisha malengo hayo ukiwa peke yake. Yaangalie malengo yako yana husu nini kisha baada ya hapo jiulize je, ni mtu gani au watu gani  ambao wanaweza kunisaidia kukamilisha malengo haya.

Kwa kujua watu ambao watakusaidia kukamilisha malengo yako itakusaidia sana kushirikiana nao kwa ukamilifu na kwa ubora wa hali ya juu hadi kufikia mafanikio yako. Tambua na elewa sio kwa sababu malengo ni yako, hivyo unatakiwa kuyakamilisha mwenyewe, hapana. Tafuta kile unachokosa, kisha omba msaada.

6. Kuwa chanya wakati wote.
Kuna wakati tunapokuwa tunajiwekea malengo huwa tunakutana na changamoto nyingi sana ambazo zinatukatisha tamaa. Sasa hali hii inapokutokea ni vyema ukajitahidi ukawa chanya wakati wote. Acha kukataa wala kujiona hufai, endelea kusonga mbele kati kati ya changamoto hizo ulizonazo wewe.

Kuwa chanya wakati unatafuta mafanikio inalipa sana. Tuchukulie kwa mfano unafanya biashara halafu ukapata hasara, hapo unafanyaje? Utaacha au itakuaje? Jibu ni kuendelea  na safari ya mafanikio kwa kutambua kwamba hiyo nayo ni hatua ya mafanikio pia. Ndiyo maana tunasema ni muhimu na lazima kuwa chanya ili kuyafikia mafanikio yako.

 7. Kuwa tayari kuyapitia malengo yako kila wakati.
Pamoja na kwamba umejwekea malengo vizuri, umejitoa kabisa kwenye malengo hayo, lakini hutakiwi kusahau kabisa kuyapitia malengo yako. Ni muhimu kuyapitia tena na tena malengo kwa kutambua wapi ulipofikia, nini kinachokukwamisha na ufanye nini ili uweze kusogea hapo ulipo kwa kasi zaidi.

Watu wengi wenye mafanikio wanayapitia malengo yao. Wanapita malengo yao asubuhi, wanapitia malengo yao mchana, wanapitia malengo yao jioni. Picha kamili ya malengo yao inakuwa ipo kichwani mwao tayari. Hiki ndicho kitu ambacho unatakiwa ukifanye hata wewe. Pitia malengo yako kila wakati ili yaumbieke vizuri na itakusaidia kuyakamilisha.

8. Jifunze kufurahia mafanikio kila hatua unayopitia.
Pamoja na kujiwekea malengo yetu makubwa, lakini kumbuka kuna yale malengo yetu madogo madogo ambayo huwa tunayashinda. Inapotokea umefanisha jambo fulani, hata kama kwako ni dogo ni vyema ukajifunza kulifurahia. Furahia mafanikio yako siku hadi siku kwa jinsi unavyoyapata.

Hiyo itakupa nguvu ya kufanikisha mambo mengine.
Kama kweli una nia njema ya kufikia mafanikio makubwa, basi hayo mambo ni ya msingi sana katika kukusaidia kufikia malengo yako makubwa uliyojiwekea. Jukumu lako kubwa ni kuhakikisha unayaweka kwenye vitendo mambo hayo.  Na kwa kufanya hivyo basi utaweza kufikia malengo yako na kutakuwa hakuna wa kukuzuia.

Friday, 19 August 2016

Saratani ya utumbo mpana!

(Colon Cancer) SARATANI YA UTUMBO MPANA NI HATARI.

SARATANI YA UTUMBO MPANA NI HATARI

Habari wadau,
Mnaweza shangaa leo kuja na uzi huu wa Saratani ya Utumbo mpana, kifupi mi si tatbibu na wala sina fani yoyote ya namna hiyo, bali mambo haya yakikukuta ndo utayajua, sometime kuliko daktari mwenyewe, hasa ukiwa mtafiti wa kwanini nimepata tatizo hili ama lile, yalinikuta, haikufika kuwa saratani, labda kwa kuwa Mungu hakutaka ifike huko, lakini cha moto nimekiona, hivyo nimeona bora tuelimishane kupitia blog hii ili sote tuwe na tahadhari ya aina fulani hasa kuhusiana na magonjwa haya ya kujitakia, ndio ni ya kujitakia, yanaitwa Lifestyle Diseases ama magonjwa yasababishwayo na mitindo yetu ya maisha.

"What you eat may play a role in your risk of colon cancer. Colon cancer may be associated with a high-fat, low-fiber diet and red meat. However, some studies have found that the risk does not drop if you switch to a high-fiber diet, so this link is not yet clear.
 
Smoking cigarettes and drinking alcohol are other risk factors for colorectal cancer." kwa mujibu wa U.S National Library of Medicine

Ndio maana nikasema ni ya kujitakia, tafiti zaonesha "90% of chronic diseases come from infection of gastrointestinal" na sababu kuu ni tatizo la kukosa choo, mi nilikuwa najiona sawa tu kama sijaenda haja siku moja au mbili, nikidhani ni kawaida, kumbe nilikuwa nalundika matatizo, mtu yeyote ambaye anapata mlo walau mlo mmoja kwa siku na kupitisha siku moja au zaidi bila kupata choo anatatizo la kukosa choo, sasa je weye unaye pata milo mitatu kwa siku bila kutoa uchafu huo je wadhani waenda wapi? kitaalumu tatizo hili lajulikana kama Constipation.

Wataalamu wanasema sababu ziko nyingi ikiwa ni pamoja na:-
Kukosa mlo kamili ama kula vyakula viingi vyenye kiwango kikubwa cha wanga na mafuta,
Kula vyakula vilivyokobolewa na vilivyo changanywa na madawa ili visiharibike,
mifumo hatarishi ya maisha (Dangeraous Lifestyles) kama vile matumizi ya pombe na sigara kwa wingi,

Ukosefu wa kiwango cha kutosha cha mbogamboga na matunda katika milo yetu,
Maji yasiyo salama,
Kuvuta hewa chafu,

Hizi ni baadhi tu, na hadhari zake zaweza kuwa:-

Chakula kutomeng'enywa vizuri (poor function of digestion system)
Maumivi makali wakati wa kupata choo,
Uchafu uliokaa muda mrefu kugeuka sumu,
Bakteria wenye madhara kuzaliwa na kuathiri utumbo mpana na viungo vingine mwilini.

Hii yaweza sababisha magonjwa sugu kama:
1. Saratani ya utumbo mpana (Colon Cancer)
2. Presha (Arteriosclerisis)
3. Kuongezeka uzito (Obesity)
4. Tumbo kujaa gesi
5. Magonjwa ya Ini
6. Figo kushindwa kufanya kazi vizuri,
7. Magonjwa ya ngozi,
8. Kukakamaa kwa mishipa ya damu,
9. Kisukari,
10. Magonjwa ya moyo n.k

Tuesday, 16 August 2016

Imani potofu kuhusu afya ya kinywa na meno!

1.POTOFU: 
Kupiga mswaki mara nyingi na kwa nguvu huzuia kuoza kwa meno

UKWELI: 
Si mara ngapi unapiga mswaki na nguvu gani inatumika, suala ni unapigaje mswaki. Kupiga mswaki mara nyingi na kwa maguvu kunaweza kupelekea kukwangua sehemu ngumu ya nje ya jino, kulifanya laini na hatimaye kuuma au hata kuvunjika.

Kupiga mswaki marambili, taratibu na kwa njia sahihi ndicho kinachosaidia meno kuwa na afya

2.POTOFU: 
Huna haja ya kumuona tabibu wamenokama hujaona au kuhisi una tatizo la meno.

UKWELI:
 Kila mtu anatakiwa kumuona tabibu wa meno angalau mara mbili kwa mwaka bila kujali meno yake yanaonekana vizuri au imara kiasi gani.

Si meno yote yanayo onekana mazuri na imara ni mazima, mengine yanaweza kuwa yameoza katikamaeneo usiyoweza ona kama chini ya fizi na kwenye mizizi, si hivyo tu hata uoto mpya(neoplasm)uweza kugundulika mapema kabla ya kufanya uaribifu mkubwa kama utachunguzwa na wataalamu.

Kumbuka pia mangonjwa ya mifumo mingine kama ukimwi,kisukari na mengine mengi hujidhihirisha mapema kinywani kabla mgonjwa hajapata dalili zingine.

3.POTIFU:
Usile kitu chochote unapo kwenda kung’oa jino

UKWELI:
Njaa inaweza kukufanya uzirahi katika zoezi la kungoa jino, hofu ikichanganyika na sukari kidogo mwilini husababisha ubongo kushindwa kufanya kazi sawa sawa.

Imani hii potofu inahusishwa na sindano ya ganzi, watu wengi wanafikiri kila ganzi inatakiwa mtu awe hakula kwa muda fulani.

Hii kwa matibabu ya meno sio kweli kwani ganzi hutolewa kwenye eneo husika tu(local anaesthesia)hivyo haiathili mwili mzima.

4.POTOFU:
Usitoe jino au kufanya matibabu ya mzizi wa jino kama una uvimbe hasa usaha

UKWELI:
Kung’oa jino au matibabu ya mzizi wa jino yanasaidia kutoa nafasi/njia kwa usaha kutoka na hivyo kupona haraka pengine bila hata kuhitaji dawa(antibiotics).Yaweza kuwa kweli pale tu kama mgonjwa atukuwa na homa au hawezi fungua kinywa ambapo itabidi udhibiti homa kwanza, na kama ni kushindwa kufungua kinywa yabidi kuacha na kutibu kinacho mfanya ashindwe kufungua kinywa kwanza.

5.POTOFU:
Mama mjamzito hastahili kutoa jino mpaka atakapo jifungua

UKWELI:
Kumuacha mama mjamzito na maumivu pamoja na ugonjwa kwaweza kufanya ugonjwa kusambaa na kuingia kwenye ubongo hata kupelekea kifo cha mama na kiumbe chake. Pia maumivu makali yaweza kusababisha mimba kutoka.

6.POTOFU:
Njia ya uhakika ya kutibu jino ni kuling’oa

UKWELI:
Ziko njia nyingi na za uhakika za kutibu jino bila kungoa. Kung’oa jino kama tiba ni pale tu ambapo jino hilo haliwezi tibika kwa njia yeyote na kukaa kwake kwa weza kuleta madhara zaidi.

Kutoa jino huleta madhara mengine na meno bandia pamoja na kwamba hayawezi kurejesha kazi za meno yaliyotoka kwa kiwango halisi, lakini pia utunzaji wake ni mgumu na gharama pia. Hata hivyo kama umelazimika kupoteza meno basi meno bandia ndilo chaguo pekee.

7.POTOFU:
Kuweka dawa ya kutuliza maumivu kama aspirini kwenye tobo kunasaidia kutoa maumivu.

UKWELI:
Kama ilivyo kwa magonjwa mengine, kutuliza maumivu wakati kisababishi cha maumivu hakija shugulikiwa ni kulikuza tatizo kwa gharama.Mbali na hivyo dawa kama aspirini uunguza fizi zilizozunguka jino ulimoiweka, pia ulilainisha(weaken)na kufanya uotaji wake uwe mgumu kwani uvunjika vunjika hovyo hovyo

8.POTOFU:
Kutoa jino husababisha kifo

UKWELI:
Kuendelea kukaa na jino lililooza na halifai kuzibwa hufanya ugonjwa kusambaa na kusababisha kifo. Unaonekana kama ukweli pale tu mgonjwa anakuja hospitalini kutoa jino

9.POTOFU:
Meno mazuri urithishwa(inherited)

UKWELI: 
Eti kwa vile tu mama au baba ana meno mazuri na mazima na wewe utakuwa hivyo au kinyume chake.

Urithi unachangia kiasi kidogo sana, utunzaji wa meno vizuri na kukutana na tabibu wa meno mara kwara ndio njia muhimu ya kuweka meno na kinywa chako sawa.

10.POTOFU: 
Hakuna haja ya kuhangaika na meno ya utotoni kwani yatatoka baada ya muda wake kufika

UKWELI: 
Meno ya utotoni yasipotunzwa vizuri yanaweza kusababisha kutoka/ kutolewa kabla ya muda wake na kupelekea meno ya ukubwani kuota kwa mpangilio usiopendeza, lakini pia katika kipindi cha mchanganyiko wa meno ya ukubwani na utotoni, meno ya utotoni yaliyooza yaweza ambukiza ya ukubwani.

11.POTOFU: 
Maumivu ya meno yatajiishia yenyewe baada ya muda.

UKWELI:
Kama jino limeoza haliwezi pona kwa namna yoyote mpaka lipate tiba hata kama haliumi. Ukiendelea kulidharau ugonjwa unaweza kusambaa mpaka maeneo mengine kama ubongo, kifuani na hatimaye kusababisha kifo.

Angalizo: 
Ni asilimia tano tu kati ya wagonjwa ambao tatizo la jino limesambaa hadi kwenye ubongo ndio huweza kupona.

Take care, tunza kinywa chako!

Fanikiwa sasa!!!

JE UNAJUA KWA NINI HUFANIKIWI?
Una mizigo mingi isiyo ya lazima wala faida ambayo
umeibeba:

1.Umejipa jukumu la kuwa “mpelelezi” wa maisha ya
wengine na umesahau maisha yako!

2.Umebeba vinyongo na visasi moyoni vinavyokufanya
uwafikirie waliokuumiza zaidi kuliko kufikiria furaha na
maendeleo yako!

3. Una marafiki wengi ambao ni kama kupe, wapo
kukutumia tu na hawachangii lolote katika maendeleo zaidi
ya kujifanya ndio watu wako karibu lakini kumbe wapo kwa
maslahi yao!

4.Umeweka mbele zaidi “watu watanichukuliaje” kuliko
kuangalia maisha yako.Watu ndio wanakuchagulia aina ya
maisha unayoishi na unajilazimisha kuishi kama wao hata kama huna uwezo huo.

5.Unaongea zaidi ya kasuku lakini vitendo hakuna.Unatamani mafanikio tu moyoni lakini huna mipango ya kuyafikia.Maisha ni mipango.

6.Maisha yako yote umeyaweka kwenye mitandao ya kijamii.Huna siri hata moja!Hivyo unalazimika kuishi aina ya maisha ambayo yataendelea kufanana na yale
uliyoyaweka kwenye mitandao ya jamii kwa sababu
ukibadilika tu watasema “umefulia”

7.Kila aliyefanikiwa ni rafiki yako au utasema ni mtu wako
wa karibu na unaishia kuwasifia tu na kupiga nao picha lakini hujifunzi kutokana na mafanikio yao na wala hutumii fursa hiyo ya kujuana nao kujifunza mambo mapya.

8.Upo sahihi kila siku(you are always right). Huambiliki,
hushauriki na kila wazo atakalotoa mwenzako basi si zuri ila la kwako ndio sahihi na utataka litekelezwe hilo hilo.
Mwisho wa siku kila mtu anakukimbia hakuna wa
kukuambia “hapa umekosea” kwa sababu ya ujuaji wako.

9.Hujifunzi maarifa mapya.Mara ya mwisho kusoma kitabu ilikuwa ni “Ngoswe, penzi kitovu cha uzembe” Tena ni kwa sababu ilikuwa ni kwa ajili ya kujibia mtihani. Hujifunzi “life skills” wala ujuzi mwingine.

10.Unazurura mno mitandaoni bila faida. Kwako wewe
intaneti ni kwa ajili ya kuchati tu na kufuatilia habari za
mjini ambazo tangu umeanza kuzifuatilia hujawahi
kuingiza hata shilingi moja, zaidi unateketeza tu hela yako
ya vocha.

ISHUSHE hiyo mizigo kama kweli unahitaji kusonga mbele!       Huu ni ujumbe haumhusu mtu yeyote yule!

Have a nice moment all!

Soma uepuke saratani!

SARATANI YA MAPAFU NA DALILI ZAKE.

SARATANI au Cancer kwa lugha ya kiingereza ni moja ya magonjwa yanayowashambulia binadamu. Kuna aina nyingi ya saratani kama vile ile ya matiti (breast) , mifupa (bones) ubongo (brain), damu (Leokamia) na kadhalika.

Tutazungumzia mfululizo wa magonjwa ya saratani hizo na leo tutajadili saratani ya mapafu, ugonjwa ambao ni hatari sana kwa binadamu.

DALILI YA SARATANI YA MAPAFU
Kuna dalili nyingi za mtu ambaye amekumbwa na ugonjwa huu, moja ya dalili ya wazi ni kupatwa na kikohozi mara kwa mara.

Baadaye mtu huyo ambaye anakohoa atapata tatizo la kushindwa kupumua kwani atakuwa akifanya hivyo kwa taabu sana. Ugonjwa huu usipogundulika mapema husambaa katika tezi ambazo zipo karibu na mapafu hivyo mgonjwa kusikia maumivu makali.

Saratani hii ya mapafu pia inaweza kusambaa mpaka katika tishu nyingine kama vile kwenye ngozi laini ya mapafu na katika moyo hivyo kuzidisha hatari kwa maisha ya mtu anayeugua maradhi haya.
Baadhi ya wagonjwa wa saratani hii ya mapafu huweza kuwasababishia matatizo katika ubongo wao, hivyo kujisikia kuumwa na kichwa.

Maradhi haya baadaye huenda katika ini hivyo kumtia matatizo mgonjwa na kwa hakika hali ikifikia hivyo huwa ni hatari.
Saratani ya mapafu huwa ndiyo chanzo kikuu cha mtu kupatwa na saratani ya mifupa ikienea sehemu zote mwilini.

NINI HUSABABISHA KUUGUA MARADHI HAYA
Zipo sababu nyingi za mtu kuugua saratani ya mapafu lakini uvutaji wa sigara, bangi au dawa za kulevya ni moja ya njia ya kusababisha mtu kuugua maradhi haya japokuwa kuna baadhi ya watu huwa wanarithi ugonjwa huu.

VIPIMO
Vipimo vya kubaini kama mtu ana saratani ya mapafu au la vipo vingi, daktari anaweza kuamua kutumia kipimo kiitwacho kitaalamu CT au kipimo kingine kiitwacho X – rey ambapo mgonjwa atapigwa picha na chombo hicho sehemu ya kifuani.

Uchunguzi huo utaweza kumfanya daktari kugundua kama saratani hiyo ya mapafu ipo katika pafu moja au mapafu yote na ataweza kujua kama mgonjwa ana seli zisizo ndogo au seli ndogo na atajua kama ugonjwa huo umeenea sana mwilini au la!

TIBA
Tiba ya saratani hii hutegemea uchunguzi ambao utagundua ni kwa kiasi gani mtu ameathirika, daktari anaweza kuamua kufanya upasuaji au kwa kutumia mionzi maalum ya kutibu maradhi haya na akigundua kuwa ugonjwa umeenea sehemu mbalimbali za mwili wa mtu anaweza kutumia njia zote kwa mgonjwa mmoja.

USHAURI
Ni vema kila mtu akawa na kawaida  ya kupima afya yake kwani magonjwa mengi yanapogundulika mapema katika mwili tiba yake huwa ni rahisi kwa daktari kuutokomeza ugonjwa na pia huwa nafuu kwa mgonjwa kwa kuwa hata gharama ya tiba huwa ni ndogo.

Ni vizuri pia kwa kila familia kujua kama mna historia ya kuwa na saratani ya aina yoyote na unapofanyiwa uchunguzi daktari kumfahamisha jambo hilo kwani kufanya hivyo kutafanya aangalie zaidi.

Ni wazi mtu ambaye familia yake imewahi kutoa mtu aliyeugua saratani ina nafasi kubwa ya kupata ugonjwa huu kuliko mtu ambaye familia yake haijawahi kuugua maradhi haya. Uonapo dalili wahi hospitali.

Have a blessed day!

Friday, 5 August 2016

Right way for Development!

RIGHT WAY FOR DELOPMENT   (RIWADE)

RIWADE, hii ni asasi isiyo ya kiserikali iliyosajiliwa mwezi Juni 2016, ikiwa na usaili namba  (ooNGO/08696) kwa lengo la kuwasaidia vijana wasio na ajira waweze kufanya kilimo, ufugaji, uvuvi wa kisasa ulio endelevu na mazingira. Na pia  kuwahusisha wakulima katika ngazi zote ili kuweza kushirikiana katika kutatua changamoto zinazokabili kilimo, ufugaji, uvuvi na mazingira kwa ujumla . Hivyo msingi wa RIWADE umejengwa kwenye mahitaji ya wakulima, wafugaji na wavuvi. RIWADE inahusisha wadau wengine kama vile washauri na watalaamu wa  vyuo vikuu, makampuni, serikali na taasisi binafsi katika kutekeleza shughuli zake. Mpango huu shirikishi unatengeneza msingi wa ubunifu ambapo, usambazaji wa elimu, utafiti na ushirikiano hujenga nguzo kuu.

 DIRA YETU. (Vission)

Kuzifikia na kuziboresha huduma za jamii ambazo zitapelekea ukuaji wa hali ya kimaisha kwa wananchi.

DHIMA YETU. (Mission)

Kutengeneza na kutoa fursa kwa watanzania wote ili waweze kupata elimu ya ujasiriamali na namna ya kutengeneza mitaji kwa ajiri ya ukuaji endelevu wa kijamii na kiuchumi.

MISINGI YETU.
Uadilifu
Uwajibikaji 
Uvumbuzi
Uaminifu 
KAULI MBIU.

"Ardhi Ni Mtaji"

    CONTACTS                                                     Managing Director
Eng. Ayubu Massau .
Head Office
P.o. box 682
Morogoro.
Tell. 0763188907

General Secretary 
Shadrack Charles Makaya
Tell. 0752817289

Project Evaluator
Elisaria Swai
Tell. 0788919510

  " IT manager"
Johnson Zablon
     Tell. 0765926368

     
Regional Managers.

Arusha Regional Manager 
Baraka S. Mchomvu
Tell. 0687176587

Lindi Regional Manager 
Shabani Zuberi
Tell. 0783728809

Ruvuma Regional Manager
Sheria Buckley
Tell. 0754424883

Kilimanjaro Regional Manager 
Shadrack Charles Makaya 
Tell. 0752817289.

Mtwara Regional Manager
Pilly Chande 
Tell. 0656635808

  Mbeya & Songwe Regional Manager
Isakwisa Banunu Mwakamoja
Tell. 0752132314.

Njombe Regional Manager
Nafiwe Miho 
Tell. 0769665206

Iringa  Regional  Manager
Vumilia J. Chacky
Tell. 0719056060

Tanga Regional Manager
Bahero Hassan Wema
Tell. 0652020297

Pwani Regional Manager
Khanifa Byamungu
Tell. 0715684196

Tabora Regional Manager
Stephen I. Nyagalu
Tell. 0757888044

Dodoma Regional Manager
Rahim Kalyango
Tell. 0717184731

Morogoro Regional Manager
Elisaria Swai
Tell. 0788919510

Mara Regional Manager
Masatu Bure Salum
Tell. 0759782429

Simiyu Regional Manager
Nkuba Kibayu
Tell. 0759919209

Mwaza & Katavi 
Regional Manager
Diana Joseph Madukwa
Tell. 0754213256

Dar es Salaam Regional Manager
Anitha Said 
Tell. 0719620644

Dar es Salaam Regional Manager
Ochieng Felix Okombo
Tell. 0654092683

Manyara Regional Manager
Batare  Mbaraka
Tell. 0769323117

Manyara Regional Manager
Fredrick Jonas 
Tell. 0682529281

Singida Regional Manager
Juma Ramadhani
Tell. 0756222314

Kigoma Regional Manager
Anton Mwita Kitereri
Tell. 0758382121

Rukwa Regional Manager Paul  Elias  Manzile
Tell.0757313953

Shinyanga Regional Manager
Elikana  Machanya
Tell. 0768011069

Geita Regional Manager
Solo manoni
Tell 0757281331

Kagera Regional Manager
Dativa Paul 
Tell: ,0765571557

Pia tunapatikana

Blog:  riwade.blogspot.com
Facebook: Riwade
Twitter:  Riwadwtz
Instagram:  Riwadetanzania
Email: riwadetanzania@gmail.com

Jinsi ya kujiamini uongeapo mbele za watu!

Mbinu Saba(7) Za Kuondokana Na Hofu Ya Kuongea Mbele Ya Kundi Kubwa!

Katika maisha zipo hofu za aina nyingi zinazomtesa binadamu. Lakini mojawapo ya hofu kubwa ambayo inasumbua sana wengi ni hofu ya kuongea mbele za watu. Hii ni hofu ambayo  huwatesa wengi sana, hasa pale wanaposikia kwamba wanakwenda kuzungumza mbele ya umati wa watu.
Wengi wanaposikia suala la kuongea mbele ya watu hali ya hofu kubwa huwaingia ndani mwao. Kutokana na hofu hiyo husababisha kwa wengine kushindwa kula vizuri, kijasho huwatoka na wakati mwingine kuhisi hata kukimbia kama uwezekano huo upo.

Mara nyingi  hofu hii huwatokea wengi sana. Na ni hali ambayo karibu kila mmoja wetu ameshawahi kukutana nayo katika maisha yake au anayo mpaka sasa. Je, inapotokea unashindwa kuongea mbele za watu huwa unachukua mikakati gani? Je, huwa unaacha kama ilivyo au ni hatua gani ambazo unachukua?

Ni muhimu kujiuliza maswali hayo na kupata majibu kwa sababu suala la kuongea mbele za watu ni la muhimu kwa kila mtu na huwezi kulikwepa. Zipo shughuli nyingi ambazo huwa zinatutaka kuwa wasemaji wakuu, hapo unafanyaje kama huwezi kumudu kuzungumza mbele ya umati? Kama kweli nia yako ni kumudu kuongea mbele za watu makala hii itakupa majibu, kivipi?

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kumudu Kuongea Mbele Ya Kundi Kubwa La Watu.

 1. Jiandae.
Ili uweze kufanikiwa vizuri kuongea mbele za watu, kwanza tambua kwa kina kile unachokwenda kukizungumza. Ikiwezekana ukiweke kwenye maandishi, kisha kifanyie mazoezi mara kwa mara. Unaweza ukafanya mazoezi hayo siku tatu kabla au hata moja.

Kwa kadri utakavyozidi kufanyia mazoezi utajikuta unakimdu vizuri na hiyo haitakupa shida sana wakati wa kuzungumza. Kwa kufanya hivyo akili yako itatulia kuliko ambavyo ungekurupuka na kwenda kuzungumza. Maandalizi ni muhimu sana ili kufanikiwa katika hili.

2. Ondoa mawazo ya kukosolewa.
Wengi wanashindwa kongea mbele za watu wengi kwa sababu ya kuogopa kukataliwa au  kuogopa kukosolewa. Wanakuwa wanaamini kwa vyovyote vile ni lazima watakosolewa. Haya ni mawazo hasi yanayowatesa sana na kuwasumbua wengi.
Lakini kwa vyovyote vile, Ukitaka kumudu kuongea mbele za watu wengi, jiamini kwanza wewe. Amini kuwa unaweza na hakuna mtu mwingine mwenye uwezo wa kuzungumza mada hiyo kuliko wewe. Acha kuamini sana katika kukoselewa, hilo litakusaidia kusimama imara.

3. Acha kufikiria watu unaongea nao.
Inaweza ikakupa shida sana kuongea mbele za watu hasa kila unapofikiria kundi kubwa la watu unaloongea nalo. Kundi hilo linaweza kuwa ni la wasomi au watu ambao wamekuzidi umri. Sasa kila ukifikiria kundi hilo unaanza kujiona kama hutaweza kuzungumza kitu.

Badala ya kufikiria kundi hilo, jitahidi kuweka mawazo yako yote kile unachokizungumza. Kiamini unachokizungumza kuwa utakizungumza kwa usahihi. Hapo ndipo mawazo yako unatakiwa uweke hapo na siyo sehemu nyingine. Hiyo itakusaidia kukuondolea hofu kwa sehemu kubwa.

4. Epuka kuongea kwa haraka.
Siri kubwa ya mafanikio ya kuongea mbele za watu ni kujifunza kongea polepole na kwa vituo. Wengi wanashindwa kumudu kuongea mbele za watu kwa sababu ya kutaka kuongea haraka haraka ili wamalize. Hii ni sumu kubwa inawafanya watu wengi washindwe kumudu kuongea mbele za watu kwa ufasaha.

Unapoongea kwa haraka kitu kinachokutokea kwanza, unakuwa unashindwa kupangilia maneno vizuri lakini pia inakuwa inakufanya ushindwe kupumua vizuri na kukufanya uongee kwa tabu. Kwa hali hiyo ni lazima kuepuka kuongea kwa haraka ili kufanikiwa kuongea mbele za watu vizuri.

5. Fikiria unaongea na mtu mmoja tu.
Sumu kubwa ya wengi kushindwa kuzungumza mbele za watu ni kuchukulia unazungumza na kundi kubwa la watu sana. Huu unaweza ukawa ndiyo ukweli halisi, lakini ili uweze kufanikiwa katika hili ni lazima kwako kujidanganya na kuchukulia kuwa unaongea na mtu mmoja.

Hapa ndipo siri ya mafanikio ilipo. Jifanye unaongea na mtu mmoja binafsi ingawa mbele yako lipo kundi kubwa. Wakati wa mazungumzo unaweza ukasisitiza jambo kwa kusema ‘unanielewa ninachosema’ badala ya kusema ‘mnanielewa ninachosema’ Hiyo itakupa nguvu ya kuondoa hofu ndani mwako.
.
6. Tuliza akili na mawazo yako.
Kwa kuwa utakuwa umeshajua kwamba unaonenda kuongea na watu wengi ni vizuri ukajua kuituliza akili yako. Kabla ya kile unachokwenda kuongea kunywa maji mengi, hiyo haitoshi unaweza ukalala zaidi usiku wke kabla ili kuiweka akili yako sawa.

Hayo yanaweza yakawa ni sehemu ya maandalizi ya kile unachokwwenda kukiongea. Ukumbuke pia akili yako inahitaji utulivu huu, ili usiwe na papara za hapa na pale. Hiyo itakusaidia kumudu zoezi zima la kuongea mbele za watu, ikiwa utakuwa makini kwa hilo.

7. Jifunze.
Tafuta namna ya kujifunza na kuweza kuongeza ujuzi wako wa kuongea mbele za watu. Unaweza ukajifunza kupitia vitabu mbalimbali au unaweza ukatafua ‘mentor’ au mshauri ambaye ameboboa katika hilo eneo na akakuongeza na kukusaidia kufikia hatua yaw ewe kuweza kumdu kuongea mbele za watu bila wasiwasi.

Haijalishi wewe ni mbovu kiasi gani wa kuongea mbele za watu. Lakini, kwa makala hii itakuwa chachu au hamasa kwako ya kuweza kukusaidia kuweza kumudu kuongea mbele za watu bila woga. Kitu kikubwa endelea kujifunza, fanyia mazoezi na mwisho wa siku utamudu hili pia na kuwa mshindi.

Tuesday, 2 August 2016

Mikojo ya walevi kutengenezewa bia!

Mikojo ya walevi kutumika kutengenezea bia!

GHENT, Ubeligiji
WATUMIAJI wa pombe sasa wataweza kupata auheni ya bei ya vinywaji hivyo, baada ya wanasayansi kugundua kifaa maalumu kitakachotumika kubadilisha mikojo ya walevi kutumika kutengenezea bia.

Kugunduliwa kwa kifaa hicho ni mkombozi kwa wamiliki wa viwanda vya pombe ambapo wataweza kupata malighafi ya kutengenezea bia kwa urahisi.

Kinatarajiwa kufungwa kwenye vyoo vya baa mbalimbali ili kurahisisha upatikanaji wa mikojo hiyo ya walevi.

Kifaa hicho ambacho kitakuwa kikitumia umeme wa jua pia kitakuwa na uwezo wa kubadili mikojo hiyo kutumika kama maji ya kunywa.

Timu ya watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Ghent nchini Ubeligiji, walisema kifaa hicho kitaanza kutumika hususan maeneo ya mijini kwenye nchi zinazoendelea.

Licha ya kuwepo kwa mashine maalum yenye uwezo wa kutibu maji machafu ikiwemo mkojo kisha kutumika kwa matumizi mengine muhimu ya binaadamu, wataalamu hao wamesema kifaa hicho walichokigundua kinauwezo zaidi wa kuyatibu maji hayo bila kutumia nguvu ya umeme.

Dk. Sebastiaan Derese, alisema kifaa hicho kitakuwa kikitunza mikojo kwenye tangi maalum ambalo litatumika kutibu kisha kutumika kama malighafi ya kutengenezea bia.

Kwa mara ya kwanza kifaa hicho kilianza kutumika kwenye tamasha la muziki ililofanyika mjini humo ambapo jumla ya lita 1000 za mikojo, zilikusanywa kisha kutengenezewa bia.

Alibainisha kuwa, bia zilizotengenezwa kupitia mikojo hiyo imewavutia wanywaji wengi hususan kwenye matamasha mbalimbali.

Je, bado utaendelea kunywa bia?