Saturday, 19 November 2016

Jipime ufahamu wako kiblia!

KWA WASOMI WA BIBLIA TUCHANGAMSHE BONGO ZETU.

1. Fundisho kuu la Biblia ni nini?
A Watu watende matendo mema
B. Wokovu kupitia kwa Yesu Kristo.
C. Wokovu ni neema tu.

2. Biblia ni tofauti na vitabu vingi. Moja ya tofauti hizo ni.
A. Ganda la juu ya biblia ni jeusi tu.
B Biblia ni kitabu kilichotafsiriwa kwa lugha nyingi kuliko kitabu chochote.
C Biblia ni kitabu kikubwa zaidi ya vitabu vingine.

3 Biblia iliandikwa kwa miaka mingapi hadi ikakamilika?
A 1500
B 1569
C 1600

4 Nani mwandishi wa Biblia.
A. Musa na manabii wengine.
B Manabii, makuhani, mitume na wafalme.
C. Roho mtakatifu kwa kuwatumia watu.

5  Vitabu vya agano la kale vimegawanyika katika makundi makuu mangapi?
A. 4
B. 2
C. 6

6. Vitabu vya agano jipya vimegawanyika ktk makundi makuu mangapi?
A. 4
B. 3
C. 6

7. Mtume Paulo peke yake ameandika vitabu vingapi kwenye Biblia?
A. 21
B. 13
C. 16

8. Mtume Yohana ameandika vitabu vingapi kwenye Biblia?
A. 1
B. 4
C. 5

9. Nani mwandishi wa kitabu cha matendo ya mitume?
A. Paulo
B. Luka
C . Timotheo

10. Kabla ya mtume Mathayo  hajaitwa na Yesu amfuate, alikua anafanya kazi gani?
A. Mtoza ushuru.
B.Mvuvi
C. Mfanya biashara.

11. Nini maana ya Biblia …………… ...................…………………………………………

12. Nini maana ya Kristo ……………………………………………………………………

13. Nini maana ya jina la Petro ……………………………………………………………………

14. Yesu alizaliwa ktk mji unaoitwaje?
……………………………………………………………………

15. Ni farisayo yupi aliyemfuata Yesu nyakati za usiku akiogopa asionekane na wayahudi?
……………………………………………………………………

16. Kulingana na injili ya Yohana, muujiza wa kwanza aliofanya Yesu ulikua ni upi?
…………………………………………………………………

17. Yesu baada ya kufufuka, alendelea kukaa duniani kwa siku ngapi?
…………………………………………………………………
18. Nani aliyembatiza kwa maji mtume Paulo?
…………………………………………………………………

19. Unafikiri ni sababu gani ilimfanya Ibrahimu aitwe " Baba wa Imani"?

20. Kwa nini  Mungu aliwachelewesha Israeli kuvuka jangwani?

******* MWISHO*****

Thursday, 17 November 2016

Chagua kunyamaza uwapo na hasira!!

          CHAGUA KUNYAMAZA

MITHALI 11:12 Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

MITHALI 17:28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.

Changamoto kubwa tuliyonayo ni kwamba tunataka kuongea kila wakati, tunataka kujibu kila tunachokisikia, kila tunachokiona tunataka kukisemea kitu.

Kuna wakati tunasikia na kukutana na mambo ambayo kiuhalisia moyo unagoma kabisa kunyamaza, unatamani ujibu, unatamani uwaambie watu yale umefanyiwa, unatamani uelezee vile umeumizwa lakini kumbe si kila jambo linatakiwa kuongelewa.

Si kila ukionacho unatakiwa kukisemea kitu. Si kila usikiacho/uambiwacho ni lazima ujibu.

Si kila ufanyiwacho ni lazima umwambie kila mtu.

MUHUBIRI 3:1 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

       Ipo nguvu katika kunyamaza

Yapo mambo ambayo tunapaswa kuongea, kusema, lakini yapo mambo ambayo tunapaswa kunyamaza kwa ajili ya usalama wa Roho zetu.

Ni kweli kuna wakati unasemwa sana vibaya, unasingiziwa, unatukanwa nk nk, lakini ni lazima ukumbuke kwamba kuna mazingira ambayo hupaswi kujibizana hata kama umeumia kiasi gani.

              Unajua ni kwanini?

Ukisemwa vibaya, ukitukanwa, ukidharauliwa lazima moyo utaghafilika, moyo ukighafilika lazima utakuwa na hasira na ghadhabu.

Ukiwa na hasira katu usitegemee kuwa utajadiliana na mtu kwa hekima.

Ukiongea utaongea katika uwepo wa hasira, ukijibu utajibu kulingana na kiwango cha hasira ulichonacho.

Sasa jiulize majibu yanayotoka kutokana na msukumo wa hasira huwa yanakuwaje?

Mazuri? Ya upole? Ya hekima? Ya unyenyekevu? I am sure jibu ni hapana.

Kama jibu ni hapana that means utaongea vitu vibaya ambavyo ni chukizo kwa MUNGU kwa sababu amesema maneno yetu na yakolee munyu (chumvi).

Sasa badala ya kuongea upumbavu na ukamkosea MUNGU kwanini usichague kunyamaza?

AMOSI 5:3 Kwa ajili ya hayo mwenye busara atanyamaza kimya wakati kama huo; kwa kuwa ni wakati mbaya.

Nimekuwa inspired sana na mwanamke Abigaili, ni kweli mumewe alikuwa na makosa, ni kweli alikuwa mlevi, lakini mwanamke huyu alijua ni wakati gani, na mazingira gani alipaswa kuongea na mumewe na alijua aongee nini. Alipomkuta mumewe yupo katika hali ya ulevi, ALINYAMAZA, alijua kuwa huu sio wakati wa kusema jambo lolote.

1 SAMWELI 25:1

Ni vyema sisi pia tukajifunza kusoma mazingira na nyakati na hali za watu zilivyo ili tujue ni wakati gani tujibu, tuongee nini na ni wakati gani tunyamaze

Kilinde kinywa, hakikisha haukiachi kinene mabaya – ZABURI 50:19.

Usipoteze marafiki na kuharibu mahusiano kwa ajili ya kinywa kibovu – MITHALI 11:9.

Ni vyema tukajifunza kujua ni neno gani tukitamka kwa wakati/hali/mazingira gani litakubaliwa –MITHALI 10:32.

ZABURI 19:14 – Bwana na akafanye maneno yetu yakapate kibali mbele zake MUNGU na mbele za wanadamu pia.

1SAMWELI 25:36

Umeumizwa, umekwazwa, umetukanwa, umedharauliwa, KATIKA MAZINGIRA YA HASIRA NA GHADHABU JITAHIDI KUNYAMAZA.

Ni kweli moyo na akili na hisia vinakusukuma kujibu, kubisha n.k, lakini elewa impact za kujibizana ukiwa na hasira na hizo ni bora ukae kimya.

AKUSHINDAE KUONGEA, MSHINDE KUNYAMAZA

          Muwe na siku njema!