Sunday, 31 July 2016

Udukuzi-programu kampeni ya Hillary Clinton

Programu ya kampeni za Hillary Clinton yadukuliwa

Maafisa wa upelelezi nchini Marekani wamesema kuwa programu ya komputa inayotumiwa na jopo linalosimamia kampeni ya Bi Hillary Clinton imedukuliwa.

Mameneja wanaosimamia kampeni ya Bi Clinton walisema kuwa wadukuzi hao wameingilia mawasiliano katika kompyuta hiyo.

Awali kamati ya jopo hilo inayosimamia ukusanyaji pesa za kampeni ilisema kuwa mawasiliano yake yalikuwa yamedukuliwa.

Vyombo vya habari Marekani vinasema kuwa udukuzi huo huenda unahusika na shughuli za upelelezi za Urusi.

Shirika la upelelezi la Marekani la FBI nalo linasema kuwa linaendelea na uchunguzi kuona iwapo makundi mengi zaidi yanaendesha udukuzi huo dhidi ya kompyuta za chama cha Democratic.

Juma lililopita mtandao wa kufichua habari za siri wa Wikileaks, unaodhaniwa kuwa na uhusiano mkubwa na Urusi ulifichua barua pepe nyingi kuhusiana na chama cha Democratic.

Yaan IT ni shidaah aise!!!

Friday, 29 July 2016

Watu wasiingilie mapenzi yenu!

Fahamu mambo ya kufanya ili kuzuia watu wasiingilie mapenzi yenu

Sio mbaya kwa marafiki wa karibu au ndugu na jamaa kufahamu kushirikiana nanyi katika mapenzi yenu kama vile wakati wa sherehe au msiba. Pia sio mbaya kujuliana hali na kutambulisha mambo ya msingi yanayoendelea katika mahusiano yako wewe na mpenzi wako.

 Hata hivyo kuna wakati watu wengine wa pembeni, wawe majirani, ndugu, wazazi au marafiki wanaweza kuwa ‘sumu’ ya mahusiano yako, hasa pale unapowategemea sana kutoa msaada, maoni au maelekezo katika maisha yako ya mapenzi.  Makala hii inaeleza mambo ya msingi unayoweza kufanya ili kupunguza uwezekano wa rafiki, ndugu, jamaa, au wazazi kuwa ‘sumu’ ya mapenzi yako.

1. Udhibiti wa taarifa kwa wengine:  
Kadri unavyoelezea mahusiano yako kwa watu wengine ndivyo unavyowapa nafasi watu kutoa maoni, na hata kudhani kuwa wana dhamana ya kukuelekeza unavyotakiwa kuishi na mwenza wako.

Hivyo basi, chukua muda wa kutosha kutafakari na kufanya uchunguzi kuhusu maswala yako ya mahusiano kabla haujaanza kutafuta maoni, ushauri kwa watu wengine. Ni bora ukasoma vitabu, na makala mbalimbali, hususani zihusuzo tabia na maisha ya mahusiano, zitafakari vema ili kuona zinahusiana vipi na unayokumbana nayo katika mahusianao yako.

2. Upekee wa mambo:
 Tambua kuwa tabia ya mpenzi wako inaweza kuwa ni ya kipekee, mazingira pia ya tukio linalokufanya utake ushauri au maoni kwa wengine yanaweza kuwa ni ya kipekee, hivyo ushauri au maoni utakayopokea yanaweza yasikusaidie moja kwa moja katika suluhisho lako.

Ukitambua hili, utafanya bidii ya kujenga uwezo binafsi wa kuchambua tatizo unalokumbana nalo katika mahusiano na kutafuta suluhisho kabla ya kutegemea watu wengine.

3. Mwenye maamuzi ni wewe:
Ni kweli kuwa kuna nyakati ni muhimu kupata ushauri kutoka kwa watu wengine, na zaidi sana watu wenye uelewa sahihi na unaowaamini, hakikisha kuwa unatambua kuwa wewe mwenyewe ndio mwenye kubeba lawama ya maamuzi utakayochukua.

4. Kuwa na subira:
Usichukue maamuziya haraka katika mahusiano hususani uamuzi wa kuamua kuwashirikisha watu wengine habari ya mambo yahusuyo uhusiano wako. Unapofanya uamuzi wa kuwashirikisha wengine kwa haraka  unajinyima nafasi ya kulichunguza jambo kwa ufasaha hususani madhara yanayoweza kutokea kwa kuwaeleza wengine, au kama ni tatizo, basi kufikiria njia sahihi ambazo ungeweza  kuzitumia kupata suluhu ya tatizo.

5. Fungua njia za mawasiliano kati yenu:
Pengine chanzo cha wewe kutaka kuzungumza mambo ya ndani yanayohusu mahusiano yenu kwa watu wengine ni kwakuwa umekosa  nafasi ya kuzungumza kwa ufasaha na mwenzi wako. Tafuteni nafasi za kutosha, jengeni mazingira ya kuzungumzia mambo yenu kabla ya kutaka kuwashirikisha watu wengine.

6. Kuweni peke yenu: 

Hata kama hautaki kueleza watu kuhusu mambo yanayoendana na maisha yenu, mazingira unamoishi yanaweza kuchangia watu kutaka kuingilia mahusiano yenu –kwa kutoa maelekezo, ushauri au maoni  kuhusu muishivyo wewe na mpenzi wako.

Inapobidi hakikisha hamuishi karibu na wazazi wenu, ndugu au rafiki wa karibu. Au haufanyi kazi na mwenzi wako sehemu moja, kwani hiyo itakuwa njia rahisi sana ya watu kuona mnavyoishi.

 Inapobidi kuwa karibu na watu wengine , hakikisha mnakubaliana wewe na mwenza wako namna bora ya kuendesha mawasiliano kati yenu mbele za watu, ili msiwape nafasi ya wao  kumi‘soma’ na kisha kuanza waje waanze kutoa ‘maelekezo’ ya vile wanavyoona mnapaswa kuishi.

7. Nenda ‘darasani’ :  Kumbuka mahusiano yanahitaji sana uelewa mkubwa wa jinsi ya kufanya mawasiliano fasaha, kuelewa hisia za mwenzi wako, kutambua mbinu za kusuluhisha migogoro, na zaidi sana kufanya mipango ya muda mrefu ya uhusiano wenu.

Jizoeshe kusoma makala na vitabu mbalimbali vyenye kuboresha ufahamu wa mambo ya msingi kama hayo tuliyoeleza hapo juu.

NB: Kuweni watu wa imani, mshirikisheni MUNGU ktk ndoa yenu! Msali na kuomba.

Mikopo Elimu ya Juu.

Waombaji wa Mikopo Elimu ya juu Wafikia 69,820 Mpaka Sasa.

JUMLA ya wanafunzi 69,820 wameomba mikopo kwa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) hadi sasa ikiwa zimebaki siku tatu kufikia mwisho wa kupokea maombi hayo.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam , Mkurugenzi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa bodi hiyo, Cosmas Mwaisoga, alisema mwaka jana walioomba kupewa mikopo walikuwa 65,000, hivyo waombaji wa mwaka huu wameongezeka.

Mwaisoga alisema tofauti na awali, mchakato wa sasa wa kuomba unafanyika kwa njia ya mtandao na baada ya kutumwa kwao, watayapitia na kwa yale yenye kasoro, wahusika wataitwa ili wayarekebishe.

Alisema dirisha la uombaji wa mikopo linatarajia kufungwa Jumapili hii.

Katika hatua nyingine, alisema idadi ya wanaorejesha mikopo imeongezeka maradufu baada ya kutakiwa kufanya hivyo.

“Kwa sasa ni vigumu kutaja idadi yao kwa sababu huwa tunaitoa mwishoni mwa mwezi kwa hiyo kesho tutakuwa na idadi kamili ya waliorejesha, lakini ikilinganishwa na huko nyuma, sasa hivi mwitiko wa wanaorejesha umeongezeka,” alisema.

Mwaisoga alisema sheria inamtaka aliyekopa aanze kurejesha baada ya mwaka mmoja wa kuhitimu masomo yake, lakini anapochelewesha, kila mwaka kunakuwa na penati ya ongezeko la asilimia sita.

Thursday, 28 July 2016

Maziwa ya mende na faida zake!!!

Maziwa ya mende chanzo bora cha protini!

Mende wa Diploptera puncata hujifungua

Wengi huenda wakawa hawawezi kuwavumilia mende, hata kuwatazama pekee, lakini wanasayansi nchini India wanasema huenda mende wakatoa tumaini kwa binadamu, katika lishe.

Wamegundua kwamba chembe za protini za maziwa kwenye mende ambazo zina virutubisho„vingi ajabu”.

Wanasema vinasema kutumiwa kama tembe ama chakula chenye virutubisho vya protini kwa kiwango cha juu.

Wanasayansi katika taasisi ya sayansi ya seli katika mji wa Bengaluru, wamefanya ugunduzi huo baada ya kutafiti muundo wa chembe za protini zinazopatikana katika utumbo wa aina ya mende wajulikanao kama Diploptera puncata, ambao ndio pekee hujifungua.

Ingawa mende kwa kawaida hawatoi maziwa, mende aina ya Diploptera puncata huwa wanatengeneza aina fulani ya maziwa yenye protini kwenye utumbo, ambayo hutumiwa kulisha watoto wake.

Chembe moja ya protini hiyo inakadiriwa kuwa na kiwango mara tatu cha nguvu ya mwili ikilinganishwa na kiasi sawa cha maziwa ya nyati.

Chembe hizo zina nguvu mara nne kushinda maziwa ya ng’ombe.

“Ni chakula kamili, unapata protini, mafuta na sukari,” amenukuliwa mmoja wa watafiti waliohusika, Sanchari Banerjee, na gazeti la The Times of India.

Mende huliwa katika maeneo mengi duniani hasa Mashariki ya Mbali

Matokeo ya utafiti huo yamechapishwa katika jarida la kimatibabu la International Union of Crystallography.

Ramaswamy anasema kwa kutumia ufahamu wao wa muundo wa protini hizo, wanaweza kutumia hamira kuzalisha chembe kama hizo kwa wingi kwenye maabara.

Isitoshe, anasema muundo wa chembe hizo unaonesha matumaini kwamba zinaweza kuundwa na kutumiwa katika vidonge vya dawa.

Je, wewe utakunywa? Toa maoni yako!

Tumia hadi line 5 kwa simu moja kwa wakati mmoja!


TUMIA LAINI ZA SIMU MPAKA 5 KWA WAKATI MMOJA UKIWA NA KIFAA HIKI

Jinsi Siku zinavyozidi kwenda mbele nayo Teknolojia inazidi kukua kwa kasi sana. Kila kuchapo utapata mpya zinazojiri katika upande wa teknolojia. Tumezoea kutumia Simu zenye Laini moja ya Simu(Singe Simcard) pia hata Simu zenye laini mbili (Dual Simcard) katika Simu zetu iwe mfumo wa Android au iOS. Ulitamani hata utumie Simcard zaidi ya mbili kwenye simu yako katika simu yako kwa kuchoka kubadirisha laini na kuweka nyingine unayohitaji kuitumia lakini ukashindwa. 


Lakini Simore Mult-Sim holder wanakuletea kifaa ambacho kinauwezo wa kutumia Laini hadi 5 katika Simu moja na zote zikawa zinapatikana bila tatizo lolote. Waweza piga simu,tuma meseji au kuwasha data za internet kwa kuchagua laini uitakayo. Pia huhitaji Kuroot Simu yako kwa wale wenye mfumo wa Android katila Simu zao  Wala huhitaji Jailbreaking kwa wale wenye mfumo wa iOS kwenye Simu zao.

Gharama ya hicho kifaa ni dolla $40 ambayo ni sawa na Tsh.87,530/= . kwa maelezo zaidi Fungua website yao  Hapa 

Toa maoni yako

Ifanye Computer yako iwake au ijizime yenyewe kwa muda utakao wewe!!

IFANYE/SET KOMPYUTA YAKO IJIANZISHE YENYEWE AU KUZIMA KWA MUDA UTAKAO

Ukiwa na computer yako unaweza kuset izimime baada Muda flani. Au kuianzisha tena baada ya muda flani. Yani kwa mfano unataka kuiset izimike baada ya masaa mawili basi waweza set kwa kutumia CMD. Fuata hatua zifuatazo kuset kompyuta yako:-

1.kuipata CMD bonyeza alama ya window bila kuachia na R (WIN+R)

2. Kitatokea kibox cheupe cheupe upande wa kushoto mwisho mwa screen yako

3. Katika hilo box andika cmd.exe na ubonyeze ENTER

4.kitakuja kibox cheusi chenye maandishi meupe

5. Utakua umemaliza kuipata CMD. Ndani ya hiyo cmd andika shutdown /t 60 /s Bonyeza ENTER. 
/t=time
/s=shutdown
60 ni muda unaotaka kompyuta yako izime. 
Kumbuka muda unauweka kwa mfumo wa seconds yani ukitaka kompyuta yako izime baada ya dakika moja unaweka 60 ikiwa na maana kwamba dakika 1=60 sekunde.

KOMPYUTA KUJIANZISHA KWA MUDA UNAOUTAKA YANI KUJI RESTART/REBOOT 
Hata hivyo waweza ianzisha kompyuta yako kwa kutumia CMD kuipata cmd fuata hatua ya 1 hadi ya 4 hapo juu. Kisha andika 
shutdown /t 60 /r kisha bonyeza ENTER
/r ikiwa na maana ya restart 
Pia ukitaka ku logoff
Log off(/l)
shutdown t/ 60 /l

Ukitaka izime,logoff,restart kwa muda huo huo bila sekunde au muda uliopangwa.

shutdown/s kisha ENTER
shutdown/r Kisha ENTER
Shutdown/l kisha ENTER

**********MWISHO********
Mshirikishe na mwenzio usisahau kumwambia endelea kufuatilia maujanja zaidi

Visit my blog and learn more!

Best hackers in the world!

THE TOP 10 NOTORIOUS HACKERS IN THE WORLD.

There are many famous hackers around the world. Here we make a list of the top 10 most notorious hackers of all time.
10 Of The Most Notorious Hackers Of All Time


10. Julian Assange

Julian Assange
Today, Julian Assange is known as the creator and public face of Wikileaks, the online organization that publishes leaked government and corporate documents. But before all that, way back in the late 80’s at the young age of 16, he was known as Mendex and together with two other hackers formed International Subversives, what they consider to be an ethical hacking group.

He went on to hack into several high-profile targets such as the US Department of Defence, NASA, Lockheed Martin, just to name a few. He was eventually caught while hacking into Nortel in 1991 at the age of 20. He pleaded guilty to 35 charges. He managed to avoid heavy penalties due to perceived non-malicious intent and a disrupted childhood, caused by his mother being part of a controversial New Age group and frequently moving about.
9. John McAfee


John McAfee Source : Flicker.com
Credit : Flicker.com
To get back at the Belize government for seizing his property, McAfee hacked all of the computers from bureaucracies to prove that the government was corrupt.
8. James Kosta


James Kosta
Image Source: Youtube.com
When he was just 14, Kosta hacked military and big business computers with his partners. Some of the businesses he hacked were IBM and General Electric, along with major banks. When he was 18, he joined the Navy to work as an intelligence analyst instead of spending 45 years in prison.
7. Gary McKinnon


Gary McKinnon
Image Source : yaabot.com
McKinnon is a Scottish hacker who, between 2001 and 2002, got access to 97 United States military networks. He hacked the military to try to prove that UFOs exist. The U.S. was unable to extradite him.
6. Adrian Lamo


Adrian Lamo
Image Source : Wikipedia.com
Lamo is known as the ‘homeless hacker’. In 2002, he hacked the computer at ‘The New York Times’ and was fined $65,000 and sentenced to two years probation. However, he really became hated because he turned in Chelsea Manning. Manning had leaked United States Army documents.
5. Jonathan James


Jonathon James
Image Source : alchetron.com
James was 15 years old when he earned the hacker nickname ‘Comrade’. In 1999, he hacked into the Department of Defense. He also hacked into the Miami-Dade school system and Bell South. When he hacked into the Department of Defense, he had access to the source code that operated the International Space System as well as other important information. He was later sentenced to probation and house arrest. On May 18, 2008, he died from a self-inflicted gunshot wound, which followed his being investigated for a massive hacking attack in 2007 that he said he was not involved with. He wrote in his suicide note that he thought he was going to be prosecuted for new crimes he didn’t commit.
4. Jeanson James Ancheta


Jeanson James Ancheta
Image Source : complex.com
Ancheta used a computer worm called ‘rxbot’ in 2004 to control 500,000 computers, including U.S. military computers, to take down major websites. He was caught in 2005 and had to serve 60 months in prison, pay back $16,000 and give up $58,000 he earned from his hacking services.
3. Kevin Poulsen


Kevin Poulsen
Image Source : Facebook.com
Kevin Poulsen, known as Dark Dante in the hacker community, specialized in hacking phone systems, particularly radio stations. This talent allowed only calls originating from his house to make it through to the station, assuring him of wins in listener radio contests. His iconic 1991 hack was a takeover of all of the telephone lines for the Los Angeles KIIS-FM radio station, guaranteeing that he would be the 102nd caller and win the prize of a Porsche 944 S2. The bold Poulsen was wanted by the FBI for federal computer hacking at the same time he was winning the Porsche and $20,000 in prize money at a separate station. Poulsen spent 51 months in a federal prison, the longest sentence of a cyber criminal at that time. Once he got out, he was banned from using computers and the internet for three years.
2. Kevin Mitnick


Kevin Mitnick
Image Source : Flickr.com
Kevin David Mitnick is one of the most notorious hackers of the 20th century. Mitnick started hacking when he was 15. He hacked into big companies like IBM, Pacific Bell, Motorola and Nokia. He got involved in several computer and communications-related crimes and even became one of the most wanted computer criminals in the United States.He was arrested in 1995 and served one year with three years of supervised release. He continued hacking and went on the run for about three years. In 1999, he was sentenced to four years in prison. Today, he is a security consultant and has written two books.
1. Michael Calce


Michael Calce
Image Source : Flickr.com
At the start of the millennium, Calce launched denial-of-services attack against Yahoo!, Amazon, eBay, CNN and Dell. He was sentenced to eight months of open custody in 2001. He was also given a small fine and wasn’t allowed to use the internet. He was in high school at the time of the attacks.

Tatua tatizo la Playstore!

Jifunze kutatua tatizo la kushidwa kupakua (Download) App toka Google Playstore.

Kunamara nyingine unaweza kukuta simu yako inashidwa kupakua (Download) App toka Google Play na kukuonesha ujumbe wa “Error 491” jifunze jinsi ya kutatua tatizo hili kwa kufata hatua zifuatazo.

Njia ya kwanza ya kufata ni kwakufuta cache zote zilizopo kwenye Google Play. fata hatua hizi.

Fungua kitufe cha  “Settings” kutoka kwenye simu yako.
Tafuta kitufe kilicho andika “Apps” au  “Application Manager” hii hutegemeana na aina ya simu unayotumia
Shusha chini mpaka ukutane na chaguo liloandikwa “All apps” kisha  ubonyeze kitufe cha “Google Play Store app”

Fungua sehemu ya maelezo ya App bonyeza kitufe cha kusimamisha shuhuli zote za App hiyo ” Force stop button”
Bonyeza chaguo lililo andikwa “Clear cache”

Kwa kufanya hivyo utakuwa umetatua tatizo lako kabisa, kama bado itaonekana tatizo linaendelea jaribu kubadilisha barua pepe ya Google (Email)  unayotumia kwenye simu yako kwa kuweka barua pepe mbadala toka Gmail njia hiyo pia huondoa tatizo.

Always visit my blog and learn a lot
elisanteblog.blogspot.com

Tuesday, 26 July 2016

Mvua ya Samaki

Mvua ya samaki ilivyotingisha Thailand

Hebu vuta picha, umeamka asubuhi na kuingia barabarani kwa ajili ya kuelekea eneo lako la kazi ghafla unakutana na samaki wengi wakiwa wametapakaa kwenye lami, huku watu wakieleza kwamba samaki hao wamedondoka kutoka angani kufuatia mvua kubwa iliyonyesha usiku!
Ni jambo la ajabu si ndiyo?

Basi kwa taarifa yako, tukio kama hilo limewahi kutokea nchini Thailand. Aprili 16, 2015, wananchi wa Thailand walishuhudia tukio la ajabu la maelfu ya samaki kukutwa barabarani, huku ikielezwa walishuka na mvua iliyonyesha usiku kucha.

Habari hiyo ilisambaa kwa kasi ikisindikizwa na picha zilizokuwa zinaonesha barabara ya lami ikiwa imefurika samaki hao.

Hata hivyo, baada ya taarifa hizo kuwa zimesambaa kwa kasi ya ajabu na kuzua mshangao karibu dunia nzima, baadaye ilibainika kwamba samaki hao hawakuwa wameshuka na mvua kutoka angani.

Taarifa kutoka kwenye mamlaka zinazohusika, zilieleza kwamba samaki hao walitapakaa barabarani baada ya lori kubwa lililokuwa limebeba shehena ya samaki hao, likielekea kwenye Mji wa Guizhou Kaili, kupata hitilafu kwenye milango yake.

Taarifa ilieleza kwamba mlango wa nyuma ulifunguka bila dereva kujua, samaki wakawa wanadondoka barabarani kwa wingi ndipo watu wakazusha kwamba waliletwa na mvua kubwa iliyonyesha usiku,” ilikaririwa taarifa kutoka kwenye mamlaka zinazohusika nchini humo na kumaliza utata kuhusu ‘mvua ya samaki’.

Thursday, 14 July 2016

Faida za Maji ya Limao!

Kunywa Maji ya Limao badala ya dawa kama una matatizo kati ya haya!

Ukinywa glasi moja ya maji ya uvuguvugu yenye limao katika tumbo tupu ni zaidi ya maji katika mwili wako.

Ina manufaa sana kwa afya zetu. Limao lina vitamin C, B, antioxidant, phosphorus, protein, flavonoids, volatile oils, carbohydrates na potassium.
Mchanyanyiko huu wa limao na maji ni kinga dhidi ya bacteria, kupambana dhidi ya virusi, kuongeza mfumo wa kinga ya mwili,

na ina tabia ya kukinga dhidi ya maambukizi. Hii ni kutokana na kuwa limao lina  pectin, magnesium, bioflavonoids, vitamins,
limonene, citric acid, na calcium.

Kwa hiyo glasi moja ya limao inasaidia katika digestion, inasaidia kutoa nje maji ya ziada na sumu mwilini, na pia inatibu tatizo la kuongezeka uzito kwa haraka. Na pia ina mazingira fulani yenye alkaline, ambayo inasaidia kusawazisha pH katika mwili.

Maji ya uvuguvugu ya limao yana manufaa haya katika afya zako:

1.Inaongeza kinga ya mwili
Kinywaji hiki huongeza mfumo wa lymphatic na kuufanya ufanye kazi kwa ufanisi.Mfumo wa lymphatic unafanya kazi sambamba
na mfumo wa kinga ya mwili kwa lengo la kulinda mwili.

2.Uondoa mawe kwenye figo
Kutokana na kiwango kikubwa cha potassium, limao linaongeza kiwango cha citrate katika mkojo, na inazuia utengenezaji
wa oxalate.

3.Inatibu Mafua na Homa.
Mara zote limao linatumika kupambana na mafua pamoja na Homa. Wingi wa antioxidants na vitamin C katika limao, linasaidia kupambana na bacteria na virusi.

4.Inapunguza maumivu ya joint, na kuvimba
Maji ya limao yanapunguza uric acid katika joints, ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa kuvimba.(hasa kwenye arthritis)

5.Inarekebisha uwiano(colitis)
Colitis ni hali ya kutokuwa na uwiano sawa kati ya alkaline na acid. Glasi moja ya limao kwa kila siku itasaidia kuweka uwiano sawa kati ya acid na alkaline katika mwili. Na itashusha wingi wa acid katika mwili.

Saturday, 2 July 2016

Madhara ya Sidiria

"Ukweli kuhusu sidiria kwa wanawake"

Kwa miaka mingi wanawake wamefunzwa kuvaa sidiria ili waweze kunyanyua maziwa yao au kuyaweka katika umbile la kupendeza.

Hata hivyo, sidiria imetajwa kuwa chanzo cha maradhi ya mgongo, misuli ya kifua, maradhi ya moyo na kusababisha kwa kiasi kikubwa  ugonjwa wa fangasi chini ya matiti, inapovaliwa kwa muda mrefu.

Utafiti mpya uliofanywa na wataalamu wa afya kutoka Chuo Kikuu cha Tiba cha Besancon, Ufaransa umebaini kuwa sidiria haimsaidii mwanamke zaidi ya kumsababishia maradhi kadhaa.

Profesa Jean-Denis Rouillon ambaye ametumia miaka 15 kufanya utafiti kwa wanawake  330 alibaini kuwa sidiria zina madhara kadhaa kwa wanawake akipingana na dhana iliyojengeka kuwa sidiria ni miongoni mwa mavazi muhimu kwa kundi hilo.

Profesa Rouillon hajawakataza wanawake kuvaa sidiria bali anasisitiza kutovaa kwa muda mrefu (mfano kulala nazo) na kutovaa mapema hata kama hunyonyeshi.

Sidiria haimpi manufaa yoyote mwanamke” anasisitiza Profesa Rouillon, ambaye katika utafiti wake alibaini kuwa wanawake ambao hawavai sidiria tangu usichana, wana maziwa imara yaliyozungukwa na misuli kakamavu kuliko wanaopendelea kuvaa nguo hiyo ya ndani.

Anasema kwa kiasi kikubwa binti anayeanza kuota maziwa anapovaa sidiria husababisha maziwa kuanguka mapema kuliko binti ambaye hatavaa sidiria.
Profesa huyo ambaye alianza kufanya utafiti tangu mwaka 1997 anasema alitumia rula na vifaa vingine kufanya utafiti huo na aligundua kuwa kuna tofauti ya milimita saba za urefu na msimamo wa maziwa kwa wasiovaa sidiria.

Sidiria imekuwa kama tegemeo pale tu mwanamke anapoanza kuota maziwa, ina maana kwamba misuli inayobeba maziwa haitumiki na badala yake sidiria inachukua wajibu huo na hivyo misuli hiyo husinyaa kwa kukosa kazi” anasema

Anasema si kweli kuwa mwanamke asiyevaa sidiria maziwa yake huanguka bali huwa na ngozi nzuri zaidi katika viungo hivyo, huwa huru na matiti huwa katika umbile zuri zaidi.

Katika ushauri wake wa majumuisho ya utafiti huo Profesa huyo alisema: “Ni dhana potofu kudhani kuwa sidiria ni msaada kwa wanawake, ninachowashauri wanawake ni kutotegemea zaidi sidiria.”

Utafiti mwingine kama huu ulifanyika  Aprili 2012, nchini Uingereza  na Dk Nicholas Ericson  ambaye alibaini kuwa wanawake wanaovaa saizi kubwa ya sidiria wapo hatarini kupata saratani ya maziwa.

Gazeti la ‘Bussiness Week’ la nchini Marekani liliwahi kuandika ripoti kuwa viwanda vinavyotengeneza sidiria nchini humo vinapata mapato ya zaidi ya dola bilioni 11 (sawa na trilioni 17 na bilioni 600 Tsh)

Hata hivyo tafiti nyingine ziliwahi kufanyika na kugundua kuwa wanawake wasiovaa sidiria wakati wa mazoezi wamo hatarini kuharibu matiti yao.
Cletus Kiwale, Daktari Bingwa wa magonjwa ya wanawake anasema hajawahi kusikia iwapo sidiria ina madhara kwa mwanamke.
Sidhani, labda sidiria inayobana sana, hata hivyo suala hilo linahitaji uchunguzi wa kina” anasema Dk Kiwale.

Naye Dk Sebalda Leshabari, Mwalimu wa Ukunga katika Chuo Kikuu cha Muhimbili anasema hakuna ukweli kuwa sidiria inasababisha madhara ila tu kwa wale watakaozivaa muda mrefu.
Mtu anapovaa kwa muda mrefu lazima atapata fangasi kwa sababu ya jasho, lakini pia, hatakuwa huru anatakiwa auache mwili upate hewa” anasema

Anasema kwa wanawake wanaonyonyesha hawana budi kuvaa sidiria ili watengeneze maumbile yao ambayo wakati huo matiti yao huwa makubwa.
Mwanamke anayenyonyesha anatakiwa avae sidiria ili azuie maziwa yasimwagike na pia ukubwa wa maziwa wakati huo humfanya asiwe huru” anasema

Dk Robert Mansel, daktari wa upasuaji katika chuo kikuu cha wales, anasema wanawake wengi wenye maumivu ya mgongo, hasa wale wanaokaribia kufunga hedhi, hupata maumivu hayo wanapovaa sidiria.
Anasema wanawake waliovaa sidiria kwa miaka mingi, wanapoacha kuvaa hupata unafuu na wepesi katika miili yao.

Profesa  Mansel anasema wanawake wengi wanaopata maumivu ya mgongo na maziwa husababishwa na uvaaji wa sidiria.
Hakuna utafiti uliowahi kufanyika na kubaini iwapo sidiria ina manufaa yeyote kiafya kwa mwanamke, lakini imekwishabainika kuwa zinaleta maumivu” anasema Dk Mansel

Dk Mansel anasema utafiti zaidi ufanyike ili kupata ukweli zaidi kuhusu madhara ya sidiria kwa wanawake.
Anitha Senkoro, mkazi wa Kigogo Dar es Salaam anasema wanawake wengi  wanavaa sidiria ili kuyaweka maziwa katika umbile zuri.
Baadhi maziwa yao hayajalala (kulegea) lakini wanavaa sidiria kwa fasheni tu na mkumbo” anasema.

Angelina Mitande,(75) Mkunga  mstaafu aliyefanya kazi katika Hospitali ya Muhimbili  miaka ya 70, anasema  zamani wanawake walivaa sidiria baada ya kujifungua ili kuhifadhi maziwa yasivuje lakini si kwa fasheni.

Unavaa sidiria ukiwa unatoka kwenda katika sherehe tu. Hatukuvaa kila wakati kama mnavyofanya siku hizi. Hata watoto wetu tuliwakataza kuva sidiria mapema” anasema

Angelina anasema kuvaa sidiria muda mrefu kunasababisha maradhi ya ngozi hasa mwanamke asipozingatia usafi.

Naishooki Kosey, Mmasai, mkazi wa Morogoro, anasema watu wa kabila hilo katu hawavai sidiria lakini maziwa yao ni madogo na mazuri.

Hata tukinyonyesha hatuvai sidiria, si jadi yetu hata kidogo. Wala mavazi yetu  hayatufanyi kukosa uhuru tusipovaa sidiria” anasema Naishooki.
Anasema binti akifundishwa kuvaa sidiria mapema, atajikuta anakuwa mtumwa wa vazi hilo hata asipovaa hawezi kutoka.

Wakati mwingine maziwa yake yana umbile zuri tu, lakini anafuata mkumbo na kuona ni nguo ya lazima kuvaa” anasema!