Tuesday, 1 March 2016

HEKA HEKA

March 1 2016 kwenye Hekaheka ya Clouds FM, Geah Habib ametuletea hekaheka iliyotokea Magomeni Dar es salaam hii ni baada ya Mtoto kupigwa na Mama anayeishi naye, tukio ambalo limepelekea mpaka majirani na mjumbe wa eneo hilo kuingilia kati.

‘Naitwa Pilli Mdidi mjumbe wa shina namba 12 nakaa mtaa wa Kiembeni nilivyopata taarifa nimeacha kupika, maana mimi ni Mama Lishe ndio nimefika hapa ndio nikaadisiwa kwamba huyu mtoto katoka ndani analia kufika juu akaanguka mpaka kuzimia ikanibidi niende kwa mama anayeishi naye kumuhoji  kwanini kampiga yule mtoto‘>>>Mjumbe

‘Mimi nafanya biashara huko Mbeya yule sio Msichana wa kazi  nilikuwa naenda kwa Mama yake ndio tukawa kama ndugu huyu Msichana natoka naye Chombe ni mdogo wangu namfundisha kupika sasa leo kuna kitu kaniudhi nikamchapa, anatabia ukimchapa anajidondosha chini‘>>>Mama aliye mpiga mtoto

No comments:

Post a Comment