Friday, 11 March 2016

INJILI YA YESU KRISTO.

Mafundisho ya Mwl. C. Mwakasege.
Dar es Salaam

SOMO: UPONYAJI KWA WALIOVUNJIKA MOYO WALIO NA HAJA YA KUPONYWA

Mistari ya kusimamia
Isaya 61:1
Luka 9:11
Yer 6:14

DAY 5/ SIKU YA 5

UTANGULIZI
Maeneo 4 lazima yapokee uponyaji huu ili uwe uponyaji kamilifu na si wajuu juu ni haya yafuatayo:-
Moyo wenyewe
Mwili wako
Kile kilichosababisha moyo kuvunjika
Chanzo cha chombo kilicho sababisha kujeruhi moyo

...Tunaendelea na kichwa kile cha MOYO ULIOVUNJIKA KUPITIA KWENYE NDOTO ULIOOTA NA MADHARA YAKE YANAYOWEZA KUTOKEA..

5⃣Baadhi ya ishara zitakazokuonyesha ya kuwa ndoto uliyoota unahitaji kuifuatilia
Kumbuka vyanzo ni vingi hivyo lazima kuwepo na ishara zikusaidie ipi ufutalie na kuishikiria

ISHARA HIZO NI KAMA:-
(I)Kuota ndoto hiyo hiyo zaidi ya mara moja
Mwz 41:1,4-5,7,32
Si lazima uote ndoto hiyo hiyo mara mbili kwa usiku mmoja, waweza ota ndo hyo siku nyingine na nyingine hiyo hiyo ama yenye maana hiyo hiyo
Maana MUNGU usema mara moja tena mara mbili na kila asemalo ulithibitisha na ulitimiza. Ayb 33:14

(II) Kukutia hofu
Dan 4:5
Angalia kama ndoto uliyoota imekutia hofu
Hii ni ishara mojawapo ya kutohidharau ndoto hiyo.

(III) Kukufadhaisha au kufadhaisha moyo wako na kukupa maangaiko moyoni
Dan 4:5
Si tu kupata hofu bali itakuletea mafadhaiko moyoni mwako

Mwz 40:5
Ndoto hizi zilikuwa halisi na kuleta mafadhaiko hata nyuso zao zilikosa furaha.
Kuna ndoto zinakuja kama taarifa tu na kuna nyingine ni vigumu kuzizuia kijuu juu tu kama ujapata msaada rohoni zitakusumbua tu.

(IV) Cheki kama uliloota limetokea katika mwili wako wakati huu
Mapambano katika ndoto ni mabaya sana na wengi uyaombea kwa maombi ya kawaida tu

(V) Kukunyima usingizi
Dan 2:1

(VI) Kuwa na hamu ya kutaka kujua tafsiri yake
Mwz 40:7-8
Walipoamka hawakuweza kutulia ndani yao walitaka kutafuta na kujua maana yake

Mwz 41:7-8
Usipuuze msukumo utakao kupata na usilizike mpaka upate na kujua maana sahihi

(VII) Ndoto kutaka kuangaisha imani yako na utumishi wako kwa MUNGU
Yer 23:25-27
Wapo watu wasemao ndoto lakini nia yao ni kuwaondoa watu kwa YESU. Kuwa nao makini

Kumb 13:1-3
Shetani pia utumia sana ndoto kuvuruga imani za watu na utumishi wao
Anatumia ndoto pia kwa kujitengenezea wafuasi na watumishi wake

Hes 12:5-6
MUNGU utumia ndoto na maono kusema na watumishi wake halisi
Na shetani utumia mlango huu huu pia
Lazima ujue kuombea vizuri mlango huu wa ndoto, usipoomba shetani atakuvuruga kweli

(VIII) Moyo wako unakuwaje unapoikumbuka ndoto uliyoota huko nyuma?
Kama hali uliyoipata wakati umeota inakukuta vile vile ukikumbuka basi jua hiyo ni ishara MUNGU anakuambia bado kuna kitu hapo hakijatatuliwa

6⃣Andika ndoto unayoiona inahitaji kufuatiliwa hatakama ni fupi kiasi gani andika
Habakuki 2:2
Andika tarehe,ulikuwa wapi, saa ngapi

7⃣Ikiwa umeota ndoto na ulipo amka umeisahau unafanyeje?
Dan 2:1-19
Msihi ROHO MTAKATIFU akukumbushe maana yeye ndiye atukumbushae yote pia endelea kumsihi MUNGU na yeye atakuotesha tena na tena

8⃣Ikiwa umeota ndoto tafsiri yake huijui ufanyeje?

(I) Omba MUNGU akupe ufahamu juu ya ndoto
Dan 1:17
Omba ufahamu ukae ndani yako ili ukiota ndoto nyingine unapata ufahamu hapo hapo
Ufahamu unakaa ndani, ni wakudumu.

(II) Mwombe MUNGU akupe tafsiri ya ndoto
Tafsiri ni tofauti na ufahamu maana tafsiri ya ndoto moja ni tofauti na ndoto nyingine
Tafsiri huja mara moja na MUNGU ndiye mtafsiri pekee. Dan 2:11, 26-28 na Mwz 40:8

(III)Uwe na NENO la Biblia la kutosha ndani yako katika hekima yote
Ayb 33:14-15
Ndoto ni neno/ujumbe/maelekezo yanayoletwa ktk picha
uja kama neno na kama ni neno basi lipo kwenye Biblia mahali
Neno lina sauti Zab 103:20
Sauti uachilia kitu unachotakiwa kupokea na kupata

Rum 10:17
Si tu kukuletea neno lazima usikie sauti iliyoko ndani ya neno kupata ufunuo, mwongozo, maelekezo, maarifa, hekima, ROHO ya uchaji na mengi mengi

Kol 3:16
Hekima hii ukusidia mahali pa kusema nani wa kumshirikisha hiyo ndoto maana si kila mtu wa kumwambia.

MIFANO YA NDOTO NA TAFSIRI ZAKE KTK BIBLIA
▶Ukiota uko darasani
Unasoma
Umechelewa mtihani
na mengi yahusuyo darasani
Soma Dan 1:1-
Mfalme aliandaa chuo na miaka ya kusoma ilikuwa 3
Darasa ni maandalizi ya hatua iliyoko mbele
Yawezekana umekwama ngazi hiyo uliyopo unahitaji kuvuka.
Muulize MUNGU umekwama eneo gani au wapi hujajiandaa kisawasawa ili uvuke.

▶Unaota mtu anakula
Zab 91:16
Amemaliza siku zake za kuishi ameshiba so ahitaji kuongeza miaka.

Isy 29:8
Moja vita uliyonayo inatoka kwenye nafsi yako we unafikiri inatoka nje
Pili walioko nje wanatumia hali ya nafsi yako kukuletea vita ya kiroho

Luk 22:14-20
Cheki nani anakulisha
Kama unalishwa na watu usiowajua au waliokufa kuna mambo haya:
I. Kuna agano unahusika nalo lililopita kwa hao watu

II. Kuna agano jipya wanataka kukuingiza

Vita hii ni mbaya sana usipopata msaada mapema uharibu hali yako na kuvuruga nyumba yako.

MUNGU AKUBARIKI MTUMISHI.

No comments:

Post a Comment